Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akitoa hotuba yake ya ufunguzi wa Semina Elimishi ya wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge na Kamati ya Uongozi katika hoteli ya White Sands jijini Dares Salaam.
Washiriki wa semina hiyo wakisikiliza mada mbalimbali zilizotolewa katika semina hiyo leo
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda(aliyevaa blauzi nyekundu akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Semina Elimishi ya wajumbe wa Tume ya Utumishi wa Bunge na Kamati ya Uongozi wakiwa katika picha ya pamoja katika hoteli ya White Sands jijini Dares Salaam.
--
NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
VIONGOZI wa Bunge wametakiwakuafuatamajukumuyaoyakazi, maadilinakufahamumipakayakeyakiutendajiilikuepushamigogoroinayowezakutokea.
Kauli hiyo ilitolewal eo naSpika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Anne Makinda wakati akifungua semina elimishi ya sikumbili ya wajumbe waTume ya Utumishi wa Bunge na Wenyeviti na Makamu Wenyeviti wa Kamati ya Uongoziwa Bunge inayoendelea katika hoteli ya White Sands jijini Dares Salaam.
Alisema kuwa Bunge ni mojawapo ya mihimili ya dola ni chombo muhimu katika uongozi na hatmaya nchi yetu, hivyo umhimu wa chombo hicho nisharti uendane na maadili ya viongozi wake.
“Ufanisi waTaasisi ya Bunge unategemea utendaji kazi wa vyombo hivi viwili kwasababu vyombo hivi viwili ndiyo washauri wakuu wa spika katika kuliongoza Bunge ,” alisema SpikaMakinda.
Aliongeza kuwa KamatiyaUongozi ndicho chombo chenye mamlaka ya kumshauri Spika kuhusu hoja na masuala mbalimbali yatakayowasilishwa Bungeni, ambapo kwa upande waTume ya Utumishiwa Bunge ndio kiungo kikuu cha Utawala na Usimamizi waHuduma mbalimbali zitolewazo kwa wabunge na watumishi wa Bunge .
Aidha Spika Makinda aliongeza kuwa vyombo hivyo viwili vinategemeana, hivyo ni muhimu kukutana ili kubadilishana mawazo na uzoefu wa namna ya kutekeleza majukumu yao kwaufanisi zaidi.
Aliwataja viongozi hao kuwa wazi na huru katika majadiliano ya mada zitakazowasilishwa.
Spika Makinda alizitaja mada zitakazowa silishwa kuwa ni tano ambazo ni maadili, uongozi na utawala bora, majukumu yaTume ya Utumishi wa Bunge naKamati yaUongozi na Mahusiano yake, taratibu za kiutendaji na mifumo ya mawasiliano serikali, nafasi ya mbunge katika uongozi, itifaki na usalama, ikiwemo mahusiano ya mihimili mitatu(Bunge, Utawala na mahakama katika uongoziwanchi.
Naye Mbungewa Jimbo la Kilindi, Beatrice Shellukindo alisema semina hiyo itawasaidia kuelewa majukumu yapi yanatakiwak utekelezwa na vyombo hivyo viwili.
0 comments:
Post a Comment