Na Francis Godwin
NAIBU spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa
Tanzania Job Ndungai amepongeza kazi nzuri inayofanywa na vyombo vya
habari nchini katika kuwafichua viongozi wanaotuhumiwa kwa Vitendo vya
ufisadi huku akitaka vyombo hivyo vya habari kuacha kuwaonea huruma wale
wote wanaojiandaa kuja kuwa viongozi wa nchi ambao wanatuhumiwa kwa
ufisadi.
Ndungai ambaye ndie alikuwa mgeni rasmi katika
maadhimisho ya kitaifa ya siku ya Uhuru wa vyombo vya habari duniani
alitoa kauli hiyo jana katika ukumbi wa Mlimani City jijini D'salaam
wakati akiwahutubia wanahabari katika Sherehe zilzoandaliwa na Misa
Tanzania na mfuko wa vyombo vya habari Tanzania ( TMF) .
Alisema
kuwa wakati wanahabari nchini wanaadhimisha siku ya Uhuru wa vyombo vya
habari ni vema wanahabari kuendelea kutathimini mwenendo mzima wa
uwajibikaji katika kuandika habari za wale wanaotuhumiwa kwa ufisadi.
Kwani
alisema kuwa pamoja na jitihada mbali
mbali vinazofanywa na vyombo vya habari katika kuandika habari za
kifisadi ila bado nguvu kubwa inatumika kuwafichua viongozi mafisadi
waliopo madarakani na kuwaonea huruma viongozi wajao jambo ambalo ni
hatari zaidi .
Alisema kinachotokea leo kwa vyombo vya habari
kuandika habari za mafisadi wa sasa waliopo madarakani na kuwaonea
huruma viongozi wajao bila kuwasema ni kutolitendea haki Taifa na siku
watakaoingia madarakani nchi itayumba zaidi.
Hata hivyo alisema
kuwa juhudi za wanahabari na vyombo vya habari nchini katika kuhabarisha
umma zimeendelea kuwa kubwa zaidi na kuwa hata shughuli za bunge
zimekuwa zikiwafikia wananchi kutokana na ushirikiano mzuri uliopo Kati
ya bunge na wanahabari.
"kweli uwajibikaji wa vyombo vya habari
kwa sasa ndio umepelekea hata kasi ya wananchi kufuatilia vikao vya
bunge kuongezeka zaidi na hata wabunge kuchangia bungeni kuongezeka japo
wanahabari mmekuwa mkituchapa sana ....Kwani mara kwa mara
mmekuwa mkipiga picha wabunge wanaosinzia japo sisi wabunge hatusemi
Kusinzia tunakuwa tunatafakari ......ila nasema kazi nzuri sana mmekuwa
mkiifanya" alisema Ndungai
Katika hatua nyingine naibu spika
huyo aliahidi kuwa bunge litaendelea na ushirikiano na vyombo vya
habari na kuwa hata miswaada miwili itakayofikishwa bungeni juu ya
mapendekezo ya Uhuru wa vyombo via habari Pindi itakavyofikishwa
bungeni
0 comments:
Post a Comment