VIONGOZI waandamizi wa Chama Cha Demokrasia
na Mendeleo CHADEMA pamoja na wanachama 15 wa chama
hicho wanatarajia kujiunga na Chama Cha NCCR Mageuzi kesho katika
ukumbi wa Hotel ya Double J jijini Mbeya. Kwa mujibu wa taarifa za chama hicho zilizotumwa kwa
njia ya ujumbe mfupi wa simu ya mkononi kwa wanahabari imedaiwa
kuwa viongozi hao wa CHADEMA watakutana na Mjumbe wa
Halmashauri Kuu ya NCCR-Mageuzi na mshauri wa mambo ya kisiasa Danda
Juju ambaye atamwakilisha, mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho
James Mbatia. Juju ambaye tayari amewasili mkoani Mbeya kwa
shughuli hiyo maalum anatarajia kuwapokea viongozi hao wa CHADEMA
ikiwa ni hatua za awali zinazodaiwa kukisambaratisha CHADEMA. Hivi karibuni aliyewahi kuwa Katibu wa Mkoa wa
CHADEMA Eddo Makata alitangaza kujiunga na NCCR-Mageuzi
baada ya
kujiuzulu kutoka CHADEMA ambapo hata hivyo viongozi wa CHADEMA
walidai kuwa walimtimua uongozi na uanachama. Wimbi la mpasuko ndani ya CHADEMA limeanza kuibuka
baada ya madai ya kutimuliwa kwa viongozi na wanachama
wa chama
hicho akiwemo, Makamu Mwenyekiti Baraza la
Vijana la
Chadema Taifa (BAVICHA)Juliana Shonza na aliyewahi
kugombea
Ubunge jimbo la Mbozi Mashariki Mtera Mwampamba. |
0 comments:
Post a Comment