ALIYEKUWA AKITAPELI WATU MTANDAONI KWA JINA LA RAFIKIELIMU,
AJULIKANA...Ni Mhitimu wa Chuo Kikuu Cha Sokoine Morogoro (
SUA ), Mkaazi wa Njombe! Zawadi Nono Ya Fedha Taslimu, Shilingi
Laki Tano ( Tsh.500,000/=) Za Kitanzania, kutolewa kwa mtu
atakaye fanikishwa kukamatwa kwa tapeli hili la mtandaoni.
Hatimaye yule tapeli sugu wa mtandaoni aliyekuwa akiwatapeli
wananchi mbalimbali kwa jina la RafikiElimu akiwahadaa
kuwapatia ajira ajulikana .
INAPOTOKA : Mnamo siku ya tarehe 11 Machi 2013, tuliripoti
kupitia blogu yetu na katika blogu mbalimbali nchini kuhusu
kuwepo kwa mtu anaye watapeli wananchi fedha kwa kutumia jina
la taasisi yetu. Tapeli huyu asiye na hata chembe ya huruma
kwa masikini wenzake, aliweka tangazo katika mtandao wa Zoom
Tanzania, mnamo mwanzoni mwa mwezi February 2013 akitangaza
nafasi za kazi z a kuvolunteer katika mikoa mbali mbali ya
Tanzania bara.
Baada ya watu kutuma maombi yao, tapeli huyo
aliyekuwa akijitambulisha kwa jina bandia la EMMANUEL ALBERT
na kwamba yeye ni HR wa RafikiElimu, aliwaambia kuwa wamepata
nafasi, na kuwatumia fomu za kujaza kisha kuwataka wamtumie
shilingi elfu Tano ( Tshs. 5,000/=) za kitanzania kwa mpesa
kwenda namba 0763906931 ( AMBAYO MBAYA ZAIDI AMEISAJILI KWA
JINA LA RAFIKIELIMU )..
Baada ya kumtumia pesa , tapeli huyo aliwatumia barua na
kuwaagiza kuripoti kazini katika taasisi mbalimbali, huku mmoja
kati yao akimuagiza aje kuripoti katika ofisi zetu.
Tulibaini juu ya uwepo wa utapeli huu mara baada ya
kutembelewa na mmoja kati ya wahanga wa utapeli huo. Dada
huyo aliye jitambulisha kwa jina la HAWA MUSSA ambaye ni
Muhitimu wa Chuo Kikuu Cha Dodoma ( 2012 ) aliripoti katika
ofisi zetu siku ya tarehe 11 Machi 2013 saa nne kamili
asubuhi na kuomba kumuona HR . Baada ya kufanya naye
mazungumzo ndipo tulipo baini kuwepo kwa utapeli unao fanyika
kwa jina la taasisi yetu. Haraka haraka tukaenda kuripoti
uhalifu huu kwenye kituo kidogo cha polisi cha Chuo Kikuu
Cha Dar Es salaam, na kukabidhiwa RB namba UD/RB/849/2013 WIZI
KWA NJIA YA MTANDAO.
Mara baada ya kupata RB moja kwa moja tulipost taarifa ya
kuwatahadharisha wananchi juu ya uwepo wa mtu anaye tapeli
watu kwa kutumia jina la taasisi yetu, huku tukiwaachia
polisi na kazi ya uchunguzi wa tukio hili la uhalifu. Wakati
polisi wakiwa bado wanaendelea na uchunguzi, siku ya Jumatatu
ya jana, tarehe 11 Machi 2013 saa sita kamili asubuhi,
tulipokea simu kutoka kwa mwakilishi wetu wa Mwanza, Dada
HADIJA SEJA akiomba tumpe namba za " MR. EMMANUEL ALBERT " (
HR wa RafikiElimu Foundation ).. Kwa kuwa tayari tulikuwa na
taarifa za jina hilo, tulimuomba dada Hadija Seja atutaarifu
kitu gani kimetokea. Dada Hadija alitupa taarifa ya kusikitisha
sana, kwamba kuna mtu mmoja aliyemtaja kwa jina moja tu la
Gerlad kutoka Arusha, amewasili jijini Mwanza kuripoti katika
ofisi za taasisi ya RESTLESS DEVELOPMENT kwa ajili ya kuanza
kazi. Mtu huyo naye ni muhanga wa tapeli huyu, na baada ya
kumtumia tapeli huyo sh. elfu tano, tapeli alimuagiza aende
kuripoti jijini Mwanza katika ofisi za RESTLESS DEVELOPMENT (
mabazo kimsingi hazipo Mwanza ). Can You imagine, huu ni
unyama wa kiwango gani, kumfanyia masikini mwenzako ushenzi
kama huo?.
Baada ya kupata taarifa hii, moja kwa moja tukaamua sisi
wenyewe kama taasisi kwenda katika ofisi za VODACOM makao
makuu zilizopo Mlimani City ili kuweza kumbaini mtu anaye
fanya unyama huu...
Tunashukuru sana Mungu, Vodacom walitupa ushirikiano wa
kutosha.. Kutoka kwenye database za Vodacom, tuligundua kwamba,
mtumiaji wa 0763906931 anaishi Njombe. Namba hii imesajiliwa
MPESA tarehe 02 February 2013, hakusajili kwa kitambulisho
chake halisi, bali kwa barua kutoka kwa Mwenyekiti wa
Serikali za Mitaa. Alisajili akiwa NJOMBE na alipokea simu
nyingi sana. Zaidi ya watu kumi waliingia katika mkenge wake
na kumtumia hizo shilingi Elfu Tano.
Mwanzoni alikuwa ana toa hela zake kwa wakala ambaye
alisajilia namba hii, lakini baadaye alisafiri na kwenda
tarafa nyingine hivyo basi kushindwa kutoa hela kwa sababu
namba ameisajili kwa jina ambalo sio lake. Hivyo basi ili
kuweza kutoa pesa ilimbidi, ajihamishie salio kutoka katika
namba 076390631 kwenda kwenye namba yake halisi ambayo ni
0765283703. Hapo ndipo tulipo weza kumbaini tapeli huyu.
Jina la huyu mtu anaitwa HASHIM MKANE na namba yake halisi
ni 0765283703. Ni mkaazi wa Njombe na amehitimu Chuo Kikuu
Cha Sokoine ( SUA ) . Aliwahi kuomba nafasi ya uwakala wa
RafikiElimu katika wilaya ya Njombe, mwezi Agosti 2012.
Baada ya kupata taarifa hizi tuliamua kutafuta mbinu za
kumkamata kirahisi,ambapo tulimtumia barua pepe, jana jioni
kisha ujumbe mfupi wa maneno ( SMS ) tukimwambia aje Dar Es
salaam kuhudhuria semina ya siku tano ya mawakala wa
RafikiElimu ( Tukamtajia na malipo ). Nadhani alistukia kwamba
huenda ameshajulikana, akatuma ujumbe mfupi wa maneno uliosomeka
:
" Nashukuru kwa taarifa hii ingawa nitashindwa kuhudhuria
kwa kuwa taarifa imechelewa kufika na ukichukulia mimi ni
mwajiliwa wa taasisi binafsi hivyo kuweza kupata ruhusa kwa
siku moja au mbili ilihali tunafanya evaluation ya mradi ni
ngumu. natumai kuhudhuria semina nyingine kama mtaiandaa "
Hapa tukajua jamaa ameshastukia mchezo na uwezekano wa
kumkamata kwa njia hiyo usingekuwa rahisi. Hivyo basi tumeamua
kuweka taarifa hii mtandaoni pamoja na picha za mtuhumiwa
huyu, ili kwa yoyote yule atakaye fanikisha kukamatwa kwa
mtuhumiwa huyu aweze kupewa zawadi nono ya shilingi Laki
Tano za kitanzania . Taarifa nyingine zitatumwa kwenye magazeti
na televisheni ili iwe rahisi kusambaza ujumbe kwa watanzania
wengi na hivyo kurahisisha kutiwa hatiani kwa dhalimu huyu .
Tafadhali upatapo ujumbe huu, wafahamishe na ndugu jamaa na
marafiki zako woote...
UKIMUONA MTU HUYU, TOA TAARIFA KATIKA KITUO CHOCHOTE CHA
POLISI KILICHO KARIBU NAWE , KISHA WASILIANA NASI KWA SIMU
0782405936. NA ENDAPO TAARIFA YAKO ITASAIDIA KUKAMATWA KWA
TAPELI HUYU, TUTAKUPATIA ZAWADI YA FEDHA TASLIMU ZA KITANZANIA
SHILINGI LAKI TANO ( Tsh. 500,000/ =)..
( KWA TAMAA YA PESA KIDOGO, AMEJIDHALILISHA, AMEDHALILISHA
TAALUMA YAKE, AMEDHALILISHA CHUO CHAKE, AMEWADHALILISHA WAZAZI,
WAKE, NDUGU , JAMAA NA MARAFIKI ZAKE, KWELI WAHENGA WALISEMA
TAMAA ILIMPONZA FISI NA MCHUMA JANGA , HUCHUMA NA WA KWA
0 comments:
Post a Comment