Home » » UNESCO YAENDESHA WARSHA YA SIKU MOJA KUJADILI RIPOTI YA HALI YA ELIMU NA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI, MAADILI NA MAHUSIANO KINGONO KWA VIJANA NCHINI

UNESCO YAENDESHA WARSHA YA SIKU MOJA KUJADILI RIPOTI YA HALI YA ELIMU NA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI, MAADILI NA MAHUSIANO KINGONO KWA VIJANA NCHINI

Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho (katikati) 
akizungumza wakati kufungua warsha siku moja ya 
mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na 
Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya
 kingono kwa Vijana nchini ambapo warsha hiyo
 imeshirikisha Taasisi mbalimbali zikiwemo AMREF,
 UNICEF, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya 
Ufundi kutoka Tanzania Bara na Visiwani, 
TGNP, Wizara ya Afya na ustawi wa Jamii na 
nyinginezo. Kushoto ni Abdoul Coulibaly wa
 UNESCO na kulia ni Mwezeshaji wa Warsha hiyo
 kutoka Chuo kishirikishi cha Elimu cha Chuo
 kikuu cha Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo.
Mwezeshaji wa Warsha hiyo kutoka Chuo 
kishirikishi cha Elimu cha Chuo kikuu cha 
Dar es Salaam (DUCE) Dr. Kitila Mkumbo akitoa 
mwongozo kwa washiriki wa warsha hiyo ambapo
 katika majumuisho yalioamuliwa kwenye warsha
 iliyofanyika leo ya kujadili Ripoti ya hali ya Elimu na
 Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya
 kingono kwa Vijana nchini yatawasilishwa katika mkutano 
wa Mawaziri utakaohusisha nchi 21 za Afrika Mashariki na Kusini.

Picha juu na chini ni National Program Officer – HIV & Sexuality 
Education Mathias Herman kutoka UNESCO
 akichambua mpango wa majukumu ya nchi za Afrika 
Mashariki na Kusini na kutoa ufafanuzi wa matokeo ya 
utafiti wa Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma za Afya ya
 uzazi, maadili na mahusiano ya kingono kwa 
Vijana nchini ambapo ameongeza kuwa nchi inatakiwa 
kujipanga kwa kusaidiwa na UNESCO pamoja na 
washirika kuongoza jitihada za kitaifa ambazo zitawawezesha 
washirika wakubwa ambao ni vijana kushiriki katika mikakati 
ya kitaifa itakayowasidia vijana nchini kujua mtazamo wao.
Pichani ni Washirki wakifuatilia uchambuzi wa Ripoti
 uliokuwa ukiwasilishwa na Mathais Herman kutoka UNESCO.
Mwakilishi kutoka Wizara ya Elimu na Ufundi stadi 
Bw. Raymond Benedict (kushoto) akikata kujua
 kuhusu mapitio ya Ripoti ya hali ya Elimu na Huduma 
za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya kingono
 kwa Vijana nchini, huduma zinazotolewa na serikali 
na nini hatma na vijana wameelewa kwa kiwango gani.
Pichani juu na chini washiriki wa warsha ya 
 siku moja iliyoandaliwa na shirika la UNESCO
 nchini wakichangia maoni yao.Pichani juu Katikati ni
 Mwenyekiti wa Asasi ya vijana ya Umoja wa Mataifa
 (YUNA) Lwidiko Edward akiwakilisha vijana na kulia ni Abdoul Coulibaly wa UNESCO
Picha juu na chini ni Washirki wakiendelea kufuatilia
 yaliyokuwa yakijiri kwenye warsha ya siku moja ya
 ya mapitio na uhakikisho wa Ripoti ya hali ya Elimu na
 Huduma za Afya ya uzazi, maadili na mahusiano ya
 kingono kwa Vijana nchini iliyofanyika leo jijini
 Dar es Salaam na kufunguliwa na Mwenyekiti wa TACAIDS Dk. Fatma Mrisho.
 
Chanzo Jestina George Blog


0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa