Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » Watu 303 wauawa katika matukio ya kishirikina nchini

Watu 303 wauawa katika matukio ya kishirikina nchini

Jumla ya watu 303 wameripotiwa kuuawa katika matukio mbalimbali yakiwemo ya kishirikina katika kipindi cha miezi sita nchini tanzania hususani katika mikoa ya shinyanga na mara.


kwa mujibu wa utafiti wa hali ya haki za binadamu nchini iliyotolewa leo na kituo cha sheria na haki za binadamu jijini dar es alaam ambapo kwa kipindi hadi june, mwaka huu, matukio hayo yameripotiwa kuongezeka.


akiwasilisha ripoti ya kutathimini taarifa za hali na haki za  binadamu  mkurugenzi wa maboresho wa kituo hicho harold sungusia amesema kwa sasa hali si nzuri nchini tanzania ambapo vitendo vya kujichukulia sheria mkononi vimekuwa vikiongezeka miongoni mwa jamii.


kuhusu suala la rasimu mpya ya katiba katika kipengele cha muungano limejitokeza katika ripoti hiyo ambapo  kituo cha sheria na haki za binadamu kimewataka wanasiasa wawaache watanzania wajadili kwa mapana katiba yao ili waweze kupata katiba iliyo bora na si bora katiba.


wakati huo huo, kituo hicho kimesema kipo katika hatua za mwisho za kumfikisha mahakamani  waziri mkuu mizengo pinda kufuatia kauli yake aliyoitoa bungeni  june 20 katika kikao cha bajeti ya  bunge.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa