Home » » Serikali, wadau wakutana kutatua ongezeko la watoto wa mitaani Dar

Serikali, wadau wakutana kutatua ongezeko la watoto wa mitaani Dar

Serikali na washirika wa masuala ya watoto nchini wamekutana kwa lengo la kutafuta mwarobaini wa kumaliza tatizo la zaidi ya watoto 5800 wanaomba barabarani mkoani dar es salaam.

mkutano huo ni sehemu ya mkakati wa kusaidia utimilifu wa ndoto za watoto hao katika maisha ikiwa ni pamoja na kudhibiti mapema madhara yanayoweza kujitokeza kwa taifa kwa miaka ijayo kufuatia ongezeko la watoto ombaomba kila wakati.

levina kikoyo ni makamu mkurugenzi wa mradi wa tuwalee pamoja wa shirika lisilo ya kiserikali (fhi) anasema asilimia 64 ya watoto wanaomba barabarani wanatamani kwenda shuleni wakati asilimia 65 hawatamani kurudi shuleni.

kwa upande wake kaimu katibu tawala msaidizi wa afya ofisi ya mkuu wa mkoa dar es salaam victoria bura amesema ipo haja kwa wazazi kutotumia watoto katika suala zima la kuomba barabarani.

naye mama wa watoto sita anayeombaomba rose james amesema ugumu wa maisha ndiyo ulichangia yeye kuombaomba licha ya watoto wake kutamani kurudi shule.

asilimia 51 ya watanzania ni watoto na kwamba inakadiliwa kuwa zaidi ya watoto milioni mbili wanaishi kwenye mazingira magumu huku milioni 1.2 kati ya watoto hao wanajihusisha na kazi ngumu ikiwemo kuomba barabarani.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa