Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » REA kutumia bilioni 881 mradi wa nishati

REA kutumia bilioni 881 mradi wa nishati


Dar es Salaam
Wakala wa nishati vijijini REA  imesaini mkataba wa shilingi bilioni 881 na wakandarasi 16 kwajili ya utekelezaji wa mradi wa nishati kwenye mikoa 24 ya tanzania bara .

Mradi huo unaotarajiwa kukamilika juni 2015 ni sehemu ya mpango mkakati wa kichocheo cha maendeleo ya taifa.

Mwenyekiti wa bodi ya nishati vijijini balozi ami mpungwe amesema  mpango huo utahusisha usambazaji umeme kwenye makao makuu ya wilaya 13 zisizo na umeme na maeneo mengine ya vijijini.

Ameongeza kuwa mpango huo umehusisha wakandarasi kutoka ndani na nje ya nchi na pia utahusisha  ujenzi wa vituo sita vya usambazaji wa umeme vitakavyojengwa tunduru, mbinga, ngara, kigoma, kasuru na kibondo.

Utekelezaji wa mpango huo ni juhudi za serikali za kufanikisha mipango ya maendeleo iliyofafanuliwa kwenye dira ya maendeleo ya taifa ya 2025 ya kufikia asilimia 30 ya nishati ya umeme kwenye maneo ya vijijini



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa