Home » » Wakili Magesa kuagwa rasmi Jumamosi 7.9.2013 Mnazi Mmoja saa 6 hadi 10

Wakili Magesa kuagwa rasmi Jumamosi 7.9.2013 Mnazi Mmoja saa 6 hadi 10


photo
Wakili Israel Magesa aliyekuwa mmiliki wa kampuni ya Mawakili ya Magesa &Co. Advocates ataagwa rasmi Jumamosi 7/9/2013 katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar Es Salaam.
Wakili Magesa ni baba  mzazi wa Phares Magesa(MNEC), Kalimba Magesa, Makongo Magesa, Yusuh (Yohana) Magesa, Rose Magesa, Salome Magesa, Rachel Magesa, Emmanuel (Sospeter )Magesa , Marehemu Elisha Magesa (RIP) na baba Mkwe wa Mrs. Haika Lawere(Mkurugenzi – Mbezi Garden Hotel), Dr. Julius Keyyu (Mkurugenzi wa Utafiti- TAWRI) na Ndg. Charanga ( Mkurugenzi – Tanzania Aviation Training College).
                                             Marehemu ameacha mjane Rhoda Magesa na wajukuu 8.                                                                 
Wakili Magesa enzi za uhai wake aliwahi kuwa Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama ya Kisutu, Katibu wa bodi na Mwanasheria Mkuu wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Msajili wa Mahakama Kuu kanda ya kusini, Mwenyekiti wa Baraza la Nyumba Dar Es Salaam, Mwenyekiti wa Amnesty International – Tanzania Chapter, Mwenyekiti wa Lions Club -Singida, pia ni mmoja wa wanasiasa waanzilishi wa siasa za vyama vingi nchini.
Enzi za uhai wake alifanya kazi ya uhakimu Mkazi mikoa ya Mbeya, Kilimanjaro, Singida, Kagera, Mtwara na Dar Es Salaam, Wakili Magesa ni miongoni mwa wanasheria waliomaliza shahada ya Sheria LLB katika Chuo Kikuu Cha East Africa miaka ya sabini mwanzoni na baadae kupata shahada ya Uzamili LLM toka Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam. Pia alipata nafasi ya kujiendeleza zaidi kimasomo katika nchi za Uingereza, Uholanzi na Sweden.
Mipango ya mazishi inafanywa nyumbani kwa Marehemu Ukonga, Majumba Sita na shughuli rasmi ya kuaga itafanyika Jumamosi tarehe 7/9/2013 kuanzia Saa 2-3 nyumbani kwa marehemu, saa 3-6 ibada kanisa la Mennonite Tanzanai-Upanga, saa 6-10 jioni shughuli rasmi ya kuaga na kutoa heshima za mwisho – Mnazi Mmoja, Dar Es Salaam na mazishi yatafanyika siku ya jumatatu  9/9/2013 kijijini Chitare, Majita, Musoma Vijijini.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa