Home » » Magufuli apiga stop usajili wa wahandisi wasiokula kiapo

Magufuli apiga stop usajili wa wahandisi wasiokula kiapo



Waziri wa Ujenzi Dk. John Magufuli amepiga marufuku utoaji wa usajili wa waandisi kwenye Bodi ya Usajili wa Waandisi nchini  ERB kabla ya kula kiapo kama sehemu ya mpango mkakati wa kupunguza vitendo vya rushwa na kusababisha ujenzi wa majengo yaliyo chini ya viwango.

Amesema kiapo kitawafanya wahandisi hao kujijengea uzalendo zaidi, hivyo kutoa agizo kwa ERB kuwaapisha waandisi 13,000 waliopo nchini.

Ni katika Mkutano wa 11 wa waandisi mbalimbali kutoka Tanzania na nchi jirani ambapo pamoja na mambo mengine wahandisi 50 waliosajiliwa na ERB waliapishwa.

Aidha amewataka waandisi hao kuongeza weledi kwenye kazi wanazopewa ili kuongeza ushindani kati yao na wahandisi toka nje ya nchi.

Mwaka 1961 Tanzania ilikuwa na Wakandarasi 2, lakini idadi hiyo imeongezeka hadi kufikia 13,000, huku bado kukiwa na changamoto ya upungufu kulingana na mahitaji huku wakitakiwa utekelezaji wa majukumu kwa wakati.

Kamati ya mioundombinu na Shirika la Viwango nchini TBS wanasema ipo haja kwa wahandisi kuhakikisha viwango sahihi vya vifaa vinavyotumika kwenye ujenzi ili kuepusha madhara yatokanayo na matumizi ya vifaa vilivyo chini ya viwango.

Zaidi ya wahandisi 1000 kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania wamekutana jijini Dar Es Salaam kujadili mambo mbalimbali yahusuyo sekta hiyo ambapo miongoni mwa mada zitakazojadiliwa ni athari za utandawazi kwa wahandisi.


0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa