Home » » CCM yaomba uvumilivu mchakato wa katiba mpya

CCM yaomba uvumilivu mchakato wa katiba mpya

Chama cha Mapinduzi CCM kimesema mchakato wa mabadiliko ya katiba unaoendelea nchini unahitaji uvumilivu wa kisiasa na kiitikadi ili kuepusha mivutano inayoweza kuchangia kupata katiba isiyokuwa na maslahi kwa watanzania.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho Nape Nnauye ametoa kauli hiyo mbele ya waandishi wa habari jijini Dar Es salaam huku akisisitiza kuwa ni lazima watanzania wajue kuwa si kila jambo linalozungumzwa litaingizwa kwenye katiba.

Mivutano baina ya vyama vya siasa, taasisi na makundi mbalimbali hapa nchini juu ya rasimu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 2013 ni miongoni mwa mambo yanayomsukuma kiongozi huyu kusema yale yaliyo moyoni mwake

Tangu ilipozinduliwa rasmi mwezi Juni mwaka huu, rasimu hiyo imekuwa gumzo hapa nchini huku vyama vya siasa vikionyesha misimamo inayokinzana hasa katika masuala nyeti likiwemo la muundo serikali, madaraka ya Rais na muungano.

Miongoni mwa matukio anayoyataja ni la hivi karibuni la wabunge wa vyama vya upinzani vya Chadema, Cuf na NCCR-Mageuzi kutoka nje ya ukumbi wa bunge kupinga muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mbadiliko ya Katiba wa mwaka 2013

Wabunge wa Bunge la Jamahuri ya Muungano wa Tanzania wanataka mjadala wa muswada huo usitishwe kwa madai kutokuwepo na usawa kiushirikishwaji, kati ya Tanzania Bara na Visiwani.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa