Dar es Salaam.Mkazi mmoja wa Mapinga mkoani
Pwani, Daniel Busiaye (58), amefariki dunia akiwa amekaa kwenye kiti cha
gari eneo la Mbuyuni wilayani Kinondoni.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura, tukio hilo lilitokea Novemba 10 mwaka huu.
Alisema mtu huyo ambaye wakati wa uhai wake alikuwa mfanyabiashara, alipanda daladala akitokea Mapinga kwenda katikati ya jiji.
Alisema gari lilipofika Mbuyuni njia panda ya
Kunduchi, mtu huyo alianguka kutoka kwenye kiti alichokuwa amekaa na
kufariki dunia papo hapo.
Wambura alisema chanzo cha kifo chake bado
hakijafahamika na kwamba mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali
ya Mwananyamala.
Alisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment