Habari
zilizotufikia hivi punde zinasema kwamba Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko
ya Katiba, Dk Sengodo Mvungi(Pichani) amefariki katika hospitali ya
MillPark huko Afrika ya kusini alkokuwa akipata matibabu.
Dk Mvungi alijeruhiwa kwa
kukatwa na mapanga kichwani Novemba 13, mwaka huu nyumbani kwake Kibamba
Msakuzi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kulazwa Taasisi ya
Mifupa ya Muhimbili (Moi) na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya Milpark,
Johannesbarg, Afrika Kusini.
: Kwa mujibu wa Hussein Bashe
Bashe “Dr Sengondo Mvungi Is No More,Taarifa zilizonifikia kutoka
Milpark Hospital Ndg yetu Mvungi Amefariki,Mnamo Majira ya Saa Tisa na
Nusu.Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi.
Wahalifu wamekatisha Uhai
wake wakati akifanya Jukumu zito kwa Ajili ya Taifa letu.Jambo hili
linaumiza sana Mungu Atalipia Uhalifu huu. poleni Tume ya Katiba,Poleni
Familia,Poleni NCCR.”Dr Sengondo Mvungi Is No More,Taarifa zilizonifikia
kutoka Milpark Hospital Ndg yetu Mvungi Amefariki,Mnamo Majira ya Saa
Tisa na Nusu.Mungu ailaze Roho ya Marehemu Mahali Pema Peponi.
Wahalifu wamekatisha Uhai
wake wakati akifanya Jukumu zito kwa Ajili ya Taifa letu.Jambo hili
linaumiza sana Mungu Atalipia Uhalifu huu. poleni Tume ya Katiba,Poleni
Familia,Poleni NCCR.
CHANZO: MO BLOG
0 comments:
Post a Comment