Home » » Jaji Chande: Jamii haijui adhabu mbadala

Jaji Chande: Jamii haijui adhabu mbadala



JAJI Mkuu wa Tanzania, Othman Chande, amesema jamii haina uelewa kuhusu adhabu mbadala inayotolewa na mahakama baada ya mtuhumiwa kukutwa na hatia ya kutumikia adhabu ya kifungo.
Jaji Chande alitoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana alipokuwa akifungua semina ya siku nane kuhusu adhabu mbadala kwa viongozi wa nchi za Afrika.
Alisema hapa nchini adhabu mbadala ilipitishwa kama sheria na kuanza kutumika mwaka 2002, lakini jamii katika mikoa na wilaya ambayo imeanza kutumiwa hawaielewi kama ipo na namna inavyofanya kazi.
Alisema mikoa 17 katika  wilaya 31 tayari imeanza kutumia adhabu mbadala ambapo katika jamii iliyozizunguka mahakama hizo inalalamika kuwa ni adhabu nyepesi.
“Jamii yetu bado ina uelewa mdogo kuhusu adhabu mbadala kwani pale inapotolewa katika mikoa na wilaya iliyoanza kutumika wanasema ni ndogo ... hawaelewi kama inamfaa mkosaji,” alisema  Jaji Chande.
Jaji Chande alisema kwa kuwa magereza hapa nchini yana wafungwa zaidi ya 35,000 kati  ya hao asilimia 30 wana makosa yanayotakiwa kutumikia kifungo cha kuanzia miaka mitano, ambao wanapaswa kupewa adhabu mbadala.
Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma kwa Jamii, Jaji Shabani Lila, alisema pamoja na adhabu hiyo kuanza kutumika, bado wana uhaba wa maofisa ustawi wa jamii ambao ndio wasimamizi wakuu wa adhabu hizo.

CHANZO;TANZANIA

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa