Home » » Viwanda kuinua uchumi nchini’

Viwanda kuinua uchumi nchini’



TANZANIA imeshauriwa kuimarisha miundombinu ya uzalishaji ikiwamo uanzishwaji wa viwanda maalumu vitakavyozalisha bidhaa kutokana na malighafi zinazopatikana nchini ili kuondokana na ongezeko la umaskini.
Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es Salaam jana na Profesa wa Uchumi, Charles Gore, wakati wa semina iliyoandaliwa na Taasisi ya Uchumi na Jamii (ESRF), iliyokuwa ikijadili jinsi ya kupunguza ongezeko la umaskini nchini.
Profesa Gore ambaye aliwahi kuwa Mkuu wa utafiti wa UNCTAD Afrika,  alisema uanzishwaji wa viwanda utasaidia kutanua wigo wa ajira ambao hivi sasa unaonekana kuwa changamoto kubwa nchini.
Alisema uchumi utakapoimarika serikali itaweza kutoa huduma za kijamii kama vile afya na elimu bure.
Hata hivyo, alisema bado kilimo kitabaki kuwa sekta muhimu pamoja na mapinduzi ya viwanda.
Mkurugenzi Mkuu wa ESRF, Dk. Hoseana Lunogelo, alisema semina hiyo iliwashirikisha wadau kutoka taasisi mbalimbali za ndani na nje.
Alisema wadau hao walijadili jinsi Tanzania inavyoweza kupunguza ongezeko la umaskini na kuleta maendeleo hususan serikali, kuwekeza zaidi kwenye sekta ya gesi na madini.

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa