Mfumo mpya unaotaka wafanyabiashara wote kuomba upya leseni za
biashara na kulipa ada kila mwaka, hautasaidia kukua kwa sekta ya
biashara nchini, wadau mbalimbali katika sekta hiyo wamebainisha.
Wadau hao wamesema mabadiliko hayo, yatasababisha
wafanyabiashara wadogo kutoweka wazi biashara zao na kuzuia ajira na
ukuaji wa sekta hiyo.
Wadau hao wamesema kutokana na uamuzi huo,
Serikali itakosa mapato, kwani wafanyabiashara wengi wataamua
kutojisajili na hivyo mzigo wa kulipa kodi kubaki kwa wafanyabiashara
wachache.
Wizara ya Viwanda na Biashara imesema hivi karibuni kwamba utoaji wa leseni bila kulipia ada umefutwa tangu Juni 30, mwaka huu.
Wadau wamesema kwamba kwa mfumo huo mpya, nchi
itakuwa na ushindani dhaifu wa biashara na itakuwa inafanywa katika
mazingira yasiyosawihi kibiashara.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wasindika Maziwa nchini, Edmund Mariki anasema Serikali imekurupuka katika uamuzi wake huo.
Anasema Serikali hivi sasa ilipaswa kuboresha
mazingira ya biashara badala ya kuchukua uamuzi huo ambao unasababisha
kikwazo kwenye ukuaji wa biashara.
Anasema kwa kuondoa au kupunguza vikwazo visivyo
muhimu katika uendeshaji wa biashara utasaidia kushawishi
wafanyabiashara wengi kuorodhesha biashara zao serikalini na kuongeza
ukusanyaji wa kodi na kutengeneza nafasi nyingi za ajira.
“Hii inasikitisha sana, tumekuwa tukishawishi
mazingira bora ya kufanya biashara, lakini serikali inarejea katika
utamaduni wa zamani ambao unakwamisha kukua kwa sekta ya biashara,”
anaeleza Mariki.
Anaeleza kuwa hana shaka na juhudi za Serikali za
kutanua wigo wa ukusanyaji kodi, lakini anafikiri kwamba kama Serikali
ikitoa leseni za biashara bure zitashawishi wafanyabiashara wengi
kujiunga na kuongeza ukusanyaji kodi.
Kwa mujibu wa Mariki, asilimia 3 tu za biashara
katika sekta ya maziwa, wajasiriamali wake wana leseni na hivyo
kutambulika rasmi.
“Badala ya kuhakikisha kwamba asilimia 97
zilizobaki zinaomba leseni, serikali inachukua hatua ambayo itawakimbiza
wengine kujiorodhesha ili kuchukua leseni, hali hii itasababisha
wengine waendelee kufanya biashara bila kujisajili.
CHANZO;MWANANCHI
CHANZO;MWANANCHI
0 comments:
Post a Comment