Dar es Salaam. Mahakama Kuu Kanda ya Dar es
Salaam, imeshindwa kusikiliza maombi yaliyofunguliwa na Kampuni ya
Uwakili ya Kings Law Chambers dhidi ya Kampuni ya kufua umeme ya Symbion
ikiomba ilipwe Dola 400,000 za Kimarekani kwa sababu Msajili,Amir Msumi
hakuwapo.
Maombi hayo yaliyotarajiwa kuanza jana,
yatasikilizwa Desemba 12,mwaka huu na Kampuni ya Kings Law Chambers
ikiwakilishwa na Wakili Emmanuel Makene inaiomba mahakama hiyo iamuru
kampuni hiyo ya Symbion iwalipe kiasi hicho cha fedha.
Kwa mujibu wa maombi hayo,Kampuni ya Kings Law
Chambers inaomba kulipwa kiasi hicho cha fedha kama sehemu ya ada ya
uwakili kwa kazi iliyoifanya ya kuiwakilisha kampuni hiyo ya kufua umeme
mahakamani wakati iliposhtakiwa na Kampuni ya Mafuta ya Mogas Tanzania
Ltd.
Katika kesi hiyo, Kampuni ya uwakili ya Kings
iliiwakilisha Kampuni ya Symbion mahakamani na kuwekeana makubaliano
kuwa kesi hiyo ikimalizika itawalipa asilimia 3 ya kiasi cha Dola 11
milioni za Kimarekani kama ada ya uwakili ambayo ni sawa na zaidi ya
Sh16 bilioni.
Kampuni ya Symbion ilipaswa kuilipa Kampuni ya
Kings Law Chambers kiasi cha Dola 460,000 kama sehemu ya ada ya uwakili
lakini ililipa kiasi cha Dola 60 milioni zikiwa bado inadaiwa Dola
400,000 Kimarekani ambayo imesababisha kuwapo kwa maombi hayo mahakamani
hapo.
Kiasi hicho cha Dola 11 milioni kilitokana na kesi
iliyowahi kufunguliwa na Kampuni ya Mogas Tanzania Ltd dhidi Symbion
kwa kuchukua mkopo wa mafuta i ya kiasi hicho cha fedha kwa kuendeshea
mitambo ya umeme ya Dodoma, Arusha na Mwanza.
Kampuni ya Symbion baada ya kuchukua mafuta kwa
mkopo yenye thamani hiyo ilishindwa kulipa,wakati ilipaswa kulipa hivyo
ilipelekea kushtakiwa.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment