Home » » KOMBE LA DUNIA KUTUA NCHINI NOV. 29

KOMBE LA DUNIA KUTUA NCHINI NOV. 29

 Kombe la Dunia la Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), linatarajiwa kuwasili nchini Novemba 29, mwaka huu.
Kombe hilo linaletwa nchini na kampuni ya vinywaji baridi ya Coca-Cola lengo ni kuwa karibu zaidi na mashabiki wa soka na tukio kubwa kuliko fainali nyingine zilizopita.
Ziara ya Kombe la FIFA la Dunia na Coca-Cola litatoa fursa kwa mashabiki zaidi ya milioni moja kushuhudia Kombe halisi la FIFA la Dunia katika nchi zao.
Akizungumza Dar es Salaam jana wakati wa hafla rasmi ya kutanganza ujio wa kombe hilo Meneja Mkazi wa Coca-Cola Tanzania Yebeltal Getachew, alisema kwamba ziara ya kombe la dunia itatoa wasaa adimu kwa maelfu ya wapenzi wa soka jijini Dar es Salaam kuliona kwa karibu Kombe halisi la dhahabu la FIFA la Dunia.
"Kupitia ziara hii na promosheni nyingine kuelekea fainali za Kombe la FIFA la Dunia 2014, Coca-Cola itasherehekea hamasa ya soka na kujaribu kuzifanya fainali zijazo kuwa shirikishi zaidi kuliko zilizopita," alisema.
Hii ni ziara kubwa na ndefu zaidi ya kombe la dunia. Ni ziara ya nchi 88 inayodumu kwa muda wa miezi tisa ambayo itajumuisha nchi 39 za bara la Latin Amerika ambako ndio bara mwenyeji wa fainali za Kombe la Dunia 2014 ilipo. Vile vile ziara hii itajumuisha nchi 50 ambazo hazijapata fursa ya kuwa wenyeji wa ziara ya Kombe la Dunia.
Ziara ya Kombe la Dunia ilianzishwa kutokana na ushirikiano wa aina ya pekee uliopo kati ya FIFA na Coca-Cola. Kampuni ya Coca-Cola ni mshirika wa FIFA wa hali ya juu na ni moja ya washirika wa FIFA wa muda mrefu.

CHANZO;MAJIRA

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa