Kamanda
wa Kikosi cha Kupambana na Kudhibiti Madawa ya Kulevya nchini, Godfrey
Nzowa amesema zaidi ya kilo 7651 za dawa za kulevya zikiwamo heroin
zimeteketezwa kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Akizungumza na NIPASHE Jumapili, Kamanda Nzowa alisema hali ya dawa
za kulevya kwa sasa ipo shwari kwani wamejiwekea mikakati ya kudhibiti
tatizo hilo na ndio maana wamefanikiwa kuwanasa watu katika maeneo
mbalimbali.
Nzowa alisema katika kipindi cha miaka mitano iliyopita
waliteketeza heroin kilo 1,596, cocain kilo tano, kubeli kilo 105, mbegu
za bhangi kilo 3,945 na bhangi kilo 2000.
Alisema kuwa mtuhumiwa wa madawa ya kulevya akisha maliza kesi
yake, aliyetoa hukumu kama ni jaji ama hakimu huamuru dawa hiyo
kuteketezwa wakati huo huo.
Kamanda Nzowa alisema dawa hizo huteketezwa kwa kushirikiana na
Mkemia Mkuu wa serikali, Maofisa wa mazingira, mpelelezi pamoja na watu
wa mahakama kwa ajili ya kushuhudia tukio hilo.
Alisema kinachoteketezwa pale ni dawa hizo na ndio maana wanawashirikisha wahusika hao ili kuweza kushuhudia suala hilo.
Pia alisema huwa hawana muda maalumu wa uteketezaji na kwamba kesi
zinapomalizika mahakamani dhidi ya dawa za kulevya ndipo huenda
kuziharibu kwenye viwanda vya saraji.
"Mwaka juzi kilo 95 za heroin, jaji aliamua zikateketezwe kwa kuwa ushahidi umemalizika na sisi tulifanya hivyo," alisema Nzowa.
Alisema mikakati yao kwa sasa ni kuhakikisha dawa hizo wanazikamata
mapema kabla ya kuwafikia walengo ili kuondoa madhara yatokanayo na
dawa za kulevya.
Pia alisema kwenye mipaka ya nchi ambayo hutumika kupitishia dawa
hizo wamewaweka raia wema ambao hutoa taarifa na kufanikiwa kuwakamata.
Kamanda alisema wale wanaojihusisha na biashara hiyo ni bora
wakaicha na kutafuta shughuli nyingine la sivyo watachukuliwa hatua kali
kwa mujibu wa sheria pale watakapokamatwa.
Alisema kuwa hadi sasa ni Watanzania wengi wamekamatwa nje ya nchi
kwa dawa za kulevya na kwamba wataendelea kupambana na suala hilo.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment