Home » » Mnyika kusikiliza kero za wananchi

Mnyika kusikiliza kero za wananchi

Dar es Salaam. Mbunge wa Jimbo la Ubungo, John Mnyika leo anakutana na wananchi wenye makazi pembezoni mwa barabara ya Morogoro waliothirika na nyongeza ya hifadhi kinyume cha sheria ya ardhi na amri ya Mahakama Kuu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya mbunge huyo, mkutano huo utakaohusisha pia kamati ya waathirika wa hifadhi ya barabara pamoja na wananchi wengine kutoka majimbo ya Ubungo, Kisarawe na Kibaha utafanyika eneo la Luguruni Makondeko.
Mkutano huo umekuja kutokana na kamati ya waathirika wa hifadhi ya barabara kumwandikia barua Mnyika na kumweleza uamuzi wa Mahakama Kuu ambayo iliamua kuwa eneo hilo wanalimiki kihalali na walipewa kwa mujibu wa sheria za nchi.
Wananchi hao wamekuwa na malalamiko ya haki zao za msingi za makazi na za kibinadamu kuvunjwa kwa maagizo kutoka kwa Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli ambayo hutekelezwa na Tanroads.
Kwa nyakati mbalimbali katika ya mwaka 2011, 2012 na 2013 yamejitokeza malumbano ndani na nje ya Bunge baina ya Mbunge Mnyika akiwakilisha wananchi na Magufuli akisisitiza msimamo wa serikali kuhusu utata wa upana wa barabara ya Morogoro na haki za wananchi.
Katika mkutano huo, mbunge atasikiliza malalamiko ya wananchi juu ya hatua ya Wizara ya Ujenzi na Tanroads bila kujali hukumu ya mahakama .
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa