Home »
» Wasomi: Kikwete amejichanganya
Wasomi: Kikwete amejichanganya

WASOMI
nchini wameshangazwa n a Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais
Jakaya Kikwete, kwa kupuuza ushauri wa wasaidizi wake wa ndani ya chama
hicho na badala yake kuamua kuendelea kuwakumbatia mawaziri wanaodaiwa
mizigo.
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti baadhi ya
wasomi walieleza kushangazwa na mabadiliko aliyofanya katika baraza lake
la mawaziri, akikataa kufanyia kazi ushauri wa msaidizi wake, Katibu
Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, kuhusiana na mawaziri mizigo.
Akizungumza
na gazeti hili Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mt. Augustino Profesa Mwesiga
Baregu, alisema CCM imejichanganya kutokana na matamshi yaliyowahi
kutolewa na katibu mkuu (Kinana) kuhusiana na maziri wote ambao
walionekana utendaji kazi wao hauridhishi.
Alisema inaonekana chama
hicho hakina sauti moja hata kwenye masuala yao ya sera hakuna maelewano
ndiyo maana walichokuwa wakieleza wananchi kwamba mawaziri mizigo
watawajibishwa, kimeshindwa kutekelezwa na Rais Kikwete.
Profesa
Baregu, alisema utekelezaji wa maamuzi au maagizo yanayotolewa ndani ya
chama hicho hayafanyiwi kazi kutokana na utekelezaji kukosa dira, hivyo
chama hicho hakiwezi kufikia malengo.
Profesa Baregu, alisema CCM
haina malengo na kama wanayo hawajatambua uelekeo wa malengo yao, ndiyo
maana wanajichanganya wenyewe.
"Ninashangaa kwani Raisi uteuzi wake
si sahihi, haiwezekani katika Wizara ya Maliasili na Utalii kumpandisha
aliyekuwa Naibu Waziri kuwa waziri kutokana na tuhuma zilizokuwepo ndani
ya wizara hiyo," alisema.
Aliongeza kuwa kutokana na Rais kuunda
tume huru ya kimahakama kwa ajili ya kuchunguza tuhuma zilizotolewa
bungeni kwa ajili ya wizara hiyo, naibu huyo alikuwepo wakati wa
Operesheni Tokomeza.
"Hakustahili kabisa kumpandisha daraja na hata
tume iliyoundwa kuchunguza hali hiyo haiwezi kupata taarifa sahihi
kutokana na tuhuma hizo kwani alitakiwa na yeye kupisha uchunguzi ili
uweze kufanyika,"alisema.
Naye Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es
Salaam, Bashiru Ally, alisema CCM inaridhika na utawala na mwelekeo
uliopo na muundo wa uchumi ulivyo badala ya kutafuta kiini cha tatizo na
kutatua haraka.
Alisema kuwa wamebaki wakihangaika na mfumo wa
ubepari wa chuma ulete, ndiyo unaosumbua kwani bado hawajajua kiini cha
tatizo wanahangaika na dalili hivyo wanatakiwa kujirekebisha.
"CCM
inatakiwa kutambua kiini cha ugonjwa kuliko kuhangaika na dalili ndiyo
maana Serikali ya Kikwete inakuwa nafukuza fukuza na kuchagua watu
wengine hali ambayo haitafuti kiini chake," alisema Ally.
Kwa
upande wake, Profesa Abdallah Safari , alisema anashangaa kuona
mwenyekiti wa CCM anapuuza ushauri wa katibu wake kwani vyama vikubwa
vinakuwa na mshikamano na kauli moja, lakini kwa CCM taswira hiyo ni
tofauti.
Alisema Katibu Mkuu wa CCM anawajibika na anatembea maeneo
mbalimbali kusikia maoni ya wananchi na kisha anayafikisha kwenye chama
na kuyatolea maamuzi, hivyo, Rais Kikwete alitakiwa kusikiliza maoni ya
wananchi na wasaidizi wake.
Pia alisema Rais inaonekana uteuzi wake
haukuwa sahihi kutokana na kumteua, Mwigulu Nchemba na Juma Nkamia,
kwani hao wamekuwa na lugha ambayo si nzuri kwa wananchi na wapinzani.
"Inaonekana
Rais Kikwete anawapenda watu wenye kauli mbaya kwa wananchi, japokuwa
katiba inamruhusu kufanya uteuzi bila kushauriwa na mtu," alisema
Profesa Safari.
Wakati huo huo, Mchungaji wa Kanisa la Anglikana la
Msalaba Mtakatifu Bagamoyo, Kelven Ngaeje, amemtaka Katibu Mkuu wa CCM,
Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya CCM NEC,
Nape Nnauye, wajiuzulu kutokana na mwenyekiti wa chama hicho kukataa
kusikiliza ushauri wao kuhusu kuwawajibisha mawaziri mizigo.
Akizungumza
kwa simu akiwa Bagamoyo jana Mchungaji Ngaeje, alisema hakuna sababu
viongozi hao kuendelea kushikilia nyadhifa hizo kwani wameshindwa
kumshauri Rais Kikwete kama walivyokuwa wameahidi kuwa kwa kupitia chama
chao watahakikisha wanamshauri Rais il kuwafuta kazi mawaziri
waliotajwa kuwa ni mizigo.
"Mbona hatujaona ahadi zao zikitimia?
Tumeshuhudia mawaziri mizigo waliokuwa wanatajwa wamerudi tena,ina maana
wao wameshindwa kumshawishi Rais ili kuwaondoa mawaziri
waliolalamikiwa."
Naye aliyekuwa Katibu Mkuu wa Chama Allience
Demokratic Change (ADC) Kadawi Limbu, amemtaka Makamu Mwenyekiti Taifa
wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Philip Mangula, Kinana na Nape Nnauye
kujipima wenyewe kutokana na ushauri wao kutozingatiwa
Chanzo;Majira
0 comments:
Post a Comment