Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), kimesema licha ya kushinda kata tatu kati ya 27 kwenye
uchaguzi mdogo wa madiwani nchini, kimetoa upinzani wa kweli kwa
kusimamisha wagombea kata ambazo hakikuwa na nguvu na kupata kura
nyingi.
Kilisema wanaolinganisha matokeo hayo ya udiwani
na mikutano ya chama hicho ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) na Operesheni
Pamoja Daima iliyofanyika hivi karibuni, wanatakiwa kuangalia kura
ambazo wagombea wa chama hicho wamepata.
Katika uchaguzi huo wa madiwani uliofanyika
Jumapili iliyopita, CCM kimeshinda kata 23, NCCR-Mageuzi kata moja na
Chadema kata tatu ambazo ni Kiborloni, Sombetini na Njombe Mjini.
Taarifa iliyotolewa na Ofisa Habari wa Chadema,
Tumaini Makene inasema watu wanalinganisha ushindi wa kata tatu
waliopata na matumizi ya helikopta tatu zilizotumika Operesheni Pamoja
Daima.
“Wanaosema hayo wamepotoka na hizo ni propaganda nyepesi,” inasema sehemu ya taarifa.
Alisema lengo la mikutano na Vuguvugu la
Mabadiliko ilikuwa ni kuzungumzia mchakato wa Katiba Mpya, uboreshaji
daftari la wapigakura, kuzungumzia rasilimali za nchi na ugumu wa maisha
unaosababishwa na sera mbovu za CCM.
“Operesheni Pamoja Daima imeibua mambo mengi;
Katiba Mpya, rasilimali za nchi na ugumu wa maisha unaowakabili wananchi
na suala la daftari la wapigakura mpaka kufikia hatua na Tume ya
Uchaguzi (NEC) kutangaza kulifanyia maboresho,” inasema.
Alisema maeneo ambayo mwaka 2010 hawakusimamisha mgombea udiwani wala mbunge, wamepata kura nyingi.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment