Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala imebaini
kwamba Idara ya Mahakama katika bajeti ya mwaka 2013/14 imepewa Sh5
bilioni tu kati ya Sh43 bilioni zilizotengwa kwa ajili ya miradi ya
maendeleo.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo William Ngeleja alisema
jana kwamba kiasi hicho ni kidogo hasa ikizingatiwa kuwa bado miezi
mitano kumalizika kwa mwaka huu wa fedha.
Alisema kitendo hicho kinakwamisha utekelezaji wa
miradi ya maendeleo na hivyo kurudisha nyuma jitihada za kutaka wananchi
kupata haki kwa wakati.
Juzi, Rais Jakaya Kikwete akizungumza kwenye Siku
ya Sheria, alitaka wadau kushirikiana katika utendaji ili kuwawezesha
wananchi kupata haki zao kwa wakati.
“Kamati inaomba Serikali iongeze speed (kasi) ya
kuipa idara hiyo fedha ili iweze kukabiliana na changamoto nyingi
zilizopo,.Kamati inasikitishwa kuwa muda uliobaki ni mfupi mwaka huu wa
fedha lakini idara hiyo imepewa asilimia 13 tu ya fedha zilizotengwa,”
alisema Ngeleja.
Alisema kamati hiyo ilikutana na Jaji Mkuu wa
Tanzania, Othman Chande na kubaini kwamba licha ya mipango mizuri lakini
tatizo kubwa ni ukosefu wa fedha.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment