Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umeanza mkakati wa kupima afya za Watanzania bila malipo nchini nzima.
                
              
Mfuko huo ambao uko nchi nzima,umekuwa ukitoa 
huduma za upimaji huo, ambapo mpaka sasa wananchi wa Mikoa ya Dar es 
Salaam, Arusha, Kilimanjaro na Zanzibar wamenufaika na mpango huo.
Meneja Mfuko wa Ilala, Christopher Mapunda alitaja
 magonjwa yatakayopimwa na wahusika kupewa ushauri wa kitaalamu katika 
mpango huo kuwa ni magonjwa yasiyoambukizwa ikiwamo kisukari, shinikizo 
la damu, uzito na urefu.a
Meneja huyo alikuwa akizungumza wakati wadau wa 
Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), waliofika katika banda 
la NHIF kwa ajili ya kupima afya zao wakati wa mkutano wa mwaka wa mfuko
 huo,
Mkurugenzi huyo alisema lengo la mpango huo ni 
kusaidia jamii kujiepusha na magonjwa hayo kwa sababu watakuwa wakitoa 
elimu kwa kuhusu afya kwa wahusika wote ambao afya zao zimeonekana kuwa 
na matatizo
“Hii itasaidia kutoa utaratibu wa kula na kufanya 
mazoezi, ili kuuweka mwili kwenye hali nzuri kiafya kwa kuwa mfuko 
unaendesha mpango huo ili kuwawezesha wananchi wajue umuhimu wa kupima 
afya zao na shughuli za NHIF,” alisisitiza.
Mkurugenzi huyo aliwataka wananchi wote kujiunga 
na mfuko huo, kwa kuwa gharama za matibabu kwa sasa zipo juu na kwamba 
siyo rahisi kwa mwananchi wa kawaida kuweza kuzimudu kwa wakati mmoja.
“Ieleweke wazi kwamba kwa sasa gharama za matibabu
 ni ghali sana, siyo rahisi kuzimudu kwa wakati mmoja, lakini ukiwa na 
NHIF kadi yako ya matibabu tayari inakuhakikishia kupata matibabu muda 
wowote’alisema
Awali baadhi ya wananchi waliopata huduma hiyo, 
waliupongeza mfuko huo kwa kuwasaidia kujua afya zao, huku wakisisitiza 
kwamba bila afya bora hakuna maendeleo endelevu katika jamii.
Chanzo;mwananchi
Chanzo;mwananchi
 
 
 
0 comments:
Post a Comment