Home » » NHIF kutoa huduma za upimaji bure nchini

NHIF kutoa huduma za upimaji bure nchini

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), umeanza mkakati wa kupima afya za Watanzania bila malipo nchini nzima.
Mfuko huo ambao uko nchi nzima,umekuwa ukitoa huduma za upimaji huo, ambapo mpaka sasa wananchi wa Mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Kilimanjaro na Zanzibar wamenufaika na mpango huo.
Meneja Mfuko wa Ilala, Christopher Mapunda alitaja magonjwa yatakayopimwa na wahusika kupewa ushauri wa kitaalamu katika mpango huo kuwa ni magonjwa yasiyoambukizwa ikiwamo kisukari, shinikizo la damu, uzito na urefu.a
Meneja huyo alikuwa akizungumza wakati wadau wa Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSPF), waliofika katika banda la NHIF kwa ajili ya kupima afya zao wakati wa mkutano wa mwaka wa mfuko huo,
Mkurugenzi huyo alisema lengo la mpango huo ni kusaidia jamii kujiepusha na magonjwa hayo kwa sababu watakuwa wakitoa elimu kwa kuhusu afya kwa wahusika wote ambao afya zao zimeonekana kuwa na matatizo
“Hii itasaidia kutoa utaratibu wa kula na kufanya mazoezi, ili kuuweka mwili kwenye hali nzuri kiafya kwa kuwa mfuko unaendesha mpango huo ili kuwawezesha wananchi wajue umuhimu wa kupima afya zao na shughuli za NHIF,” alisisitiza.
Mkurugenzi huyo aliwataka wananchi wote kujiunga na mfuko huo, kwa kuwa gharama za matibabu kwa sasa zipo juu na kwamba siyo rahisi kwa mwananchi wa kawaida kuweza kuzimudu kwa wakati mmoja.
“Ieleweke wazi kwamba kwa sasa gharama za matibabu ni ghali sana, siyo rahisi kuzimudu kwa wakati mmoja, lakini ukiwa na NHIF kadi yako ya matibabu tayari inakuhakikishia kupata matibabu muda wowote’alisema
Awali baadhi ya wananchi waliopata huduma hiyo, waliupongeza mfuko huo kwa kuwasaidia kujua afya zao, huku wakisisitiza kwamba bila afya bora hakuna maendeleo endelevu katika jamii.
Chanzo;mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa