Home » » TPCC kuanza kuzalisha umeme wake

TPCC kuanza kuzalisha umeme wake

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Kampuni ya Saruji ya Twiga (TPCC), ina mpango wa kujenga uwezo wa kuzalisha umeme wake ili kupunguza au kuondoa tatizo la nishati hiyo wakati wa uzalishaji.
Hatua hiyo inakuja ikiwa ni mwendelezo wa kiwanda hicho kuboresha mkakati wake wa biashara, kuhakikisha bidhaa ya saruji inayozalishwa kiwandani hapo inamfikia mteja kwa bei nafuu.
Akizungumza kwenye chakula cha jioni kwa wasambazaji saruji kutoka maeneo mbalimbali nchini mjini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, Mkurugenzi Mtendaji wa TPCC, Alfonso Rodriguez alisema kampuni yake imeamua kuweka mfumo mpya wa mkakati kukabiliana na ushindani wa soko.
Rodriguez alisema kampuni hiyo kila mwaka ina utaratibu wa huandaa chakula cha jioni kwa wasambazaji wake nchini, lengo likiwa ni kubadilishana mawazo na uzoefu wa biashara ya saruji nchini.
Hata hivyo, Rodriguez alipongeza hatua za Serikali inazochukua kudhibiti uagizaji saruji kwa njia za panya na kuuzwa kwa bei ya chini, kwani kitendo hicho kinasababisha ushindani usio wa haki.
Akiwasilisha ripoti ya masoko kwa wasambazaji, Rodriguez alisema Twiga Cement kama ilivyo kwa kampuni nyingine za saruji imekuwa ikikabiliana na changamoto kubwa kwa soko nchini.
Alisema changamoto hiyo inasababishwa na uagizaji na udhibiti hafifu wa saruji kutoka nje ya nchi, hususan Pakistan na tatizo la mgawo wa umeme unaopunguza uzalishaji kwa kiwango kikubwa.
Katika hafla ya mwaka huu kampuni ya Nayan Enterprises iliinuka kidedea kwa kuwa msambazaji bora wa mwaka nafasi ya pili ikichukuliwa na Mwanza Huduma Ltd ya tatu ikiwa kampuni ya VGK na Texas Hardware ikishika nafasi ya nne.
 Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa