Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (Tucta) limeeleza
kusikitishwa na utata wa wanawake wawili wenye majina yanayofanana
kuwasili katika Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodima kwa nafasi ya
ujumbe wa Bunge hilo kilisema halimfahamu Amina Mweta wa Kilimanjaro.
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake jana,
Katibu Mkuu wa Tucta, Nicholaus Mgaya alisema, mazingira ya tukio hilo
yamewatisha, hivyo kulazimika kumwandikia barua Katibu Mkuu Kiongozi,
Balozi Ombeni Sefue ili kumthibitisha mjumbe wao halali.
“ Kwa kweli tumeshtushwa na taarifa hizo za
kujitokeza mjumbe mwenye jina linalofanana na mjumbe wetu, hivyo
tumelazimika kuandika barua kwa Katibu Mkuu Kiongozi na kwa Katibu wa
Bunge ili kumthibitisha mjumbe wetu halali tunayemtambua ambaye ni Amina
Mweta kutoka mkoani Songea,” alisema Mgaya.
Alifafanua kwamba, mjumbe anayetambuliwa na Tucta
ni Amina Mweta ambaye ndiyo jina lake lilipelekwa kwa Rais ili
kufanyiwa uteuzi, likiwa pamoja na majina ya wawakilishi wa vyama
vingine vya wafanyakazi.
“ Mweta huyo tunayemtambua ana umri miaka 43 ni
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa Chama cha Wafanyakazi wa Mawasiliano na
Usafirishaji (COTWU) kutoka Songea, hivyo tunaamini kwamba viongozi hao
watatuelewa ili mjumbe huyo aendelee kushiriki kama mwakilishi wetu
halali,” alisema. Mgaya hata hivyo, alieleza kwamba tukio hilo
limewashangaza kwamba baada ya mjumbe huyo mwingine kujitokeza na kudai
kwamba alipigiwa simu na Ofisi ya Bunge na kupewa taarifa za
kuchaguliwa.
“Kinachoshangaza na kuonyesha kwamba kuna jambo
lisilo la kawaida katika tukio hili ni kwamba namba za huyo Mweta asiye
mjumbe halali zilipatikana wapi hadi wampigie simu, tunaomba vyombo
husika vichunguze suala hili kwa umakini, huu ni mchezo wa hatari fedha
ya Serikali tayari inadaiwa kutumika,” alisisitiza Mgaya.
“ Jambo lingine ni kwamba hata katika Chama cha
Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa (TALGWU) anachodai kutoka huyo Mweta wa
Kilimanjaro hawakuwa wamependekeza jina lake, bali walipendekeza Edna
Mwaigomole ambaye ni Mwenyekiti TALGWU kutoka Mbeya na Sudi Madega
Katibu wa TALGWU Dar es Salaam ambao hawakubahatika kuchaguliwa na
Rais,”alisema Mgaya.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment