Home » » Yombayomba amlilia Rais Kikwete amrudishe kazini

Yombayomba amlilia Rais Kikwete amrudishe kazini

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Bingwa wa zamani ya ngumi wa Jumuiya ya Madola kwenye uzani wa Bantam, Michael Yombayomba amemwomba Rais Jakaya Kikwete amrudishe kazini.
Yombayomba bondia pekee aliyewahi kuiletea Tanzania medali ya dhahabu ya Jumuiya ya Madola aliyasema hayo hivi karibuni katika mahojiano na gazeti hili nyumbani kwao Kibaha.
“Ninachokiomba hivi sasa ni huruma ya Rais Kikwete ili nirudishwe kazini, maisha ‘yamenipiga’ na kazi ndiyo kila kitu kwangu, hivi sasa naadhirika,” alisema Yombayomba.
Bondia huyo ambaye pia aliwahi kutwaa medali ya shaba ya michezo ya Afrika alisema amekuwa akiishi maisha magumu ya dhiki baada ya kufukuzwa kazi mwaka 2002 hadi leo na kufikia hatua ya kufanya vibarua vya hapa na pale ili kujikimu.
“Niliongea na Rais siku ya sherehe ya Kifimbo cha Malkia kwenye Viwanja vya Ikulu na kumweleza matatizo yangu, najua ana majukumu mengi, lakini kupitia gazeti la Mwananchi naomba anisaidie nirudishwe kazini,” alisema Yombayomba.
Bondia huyo alifukuzwa kazi miaka michache baada ya kupewa usajenti kutokana na kushinda medali ya dhahabu ya Jumuiya ya Madola, hata hivyo alifukuzwa ndani ya saa 24 kwa kile alichoeleza ni kuondoka kwenye kambi ya timu ya taifa na kwenda kuiaga familia yake kabla ya safari ya Uingereza kwenye michezo ya Madola ya msimu huo na kudaiwa kutoroka kambini hivyo kufunguliwa kesi ya utoro jeshini.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa