Home » » TOC yatoa tahadhari kwa vyama

TOC yatoa tahadhari kwa vyama

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Kamati ya Olimpiki Tanzania (TOC) imesema itatoa mamlaka kamati yake ya Ufundi kuteua wachezaji watakaoiwakilisha nchi kwenye Michezo ya Jumuiya ya Madola endapo vyama vya michezo vitashindwa kuwateua wachezaji wao wenye viwango hadi Jumamosi hii.
Tanzania itawakilishwa na timu za judo, ngumi, riadha, kuogelea, mpira wa meza, paralimpiki, baiskeli na kunyanyua vitu vizito kwenye michezo hiyo iliyopangwa kufanyika katikati ya mwaka nchini Scotland.
Akizungumza na Gazeti hili makao makuu ya kamati hiyo jijini jana, Katibu Mkuu wa TOC, Filbert Bayi alisema endapo vyama vitashindwa kuthibitisha idadi ya wachezaji wake kamati yao ya ufundi Jumamosi hii itachukua jukumu hilo.
“Awali vyama vilituletea majina mengi ya wachezaji tukawaambia waende na walete majina ya wale tu wenye viwango vya kushiriki madola na mwisho ilikuwa ni  leo ‘jana’ lakini hadi sasa hivi ‘ jana saa tano asubuhi’ hakuna hata chama kimoja kilichofanya hivyo,” alisema Bayi.
Alisema endapo vyama hivyo vitashindwa kupeleka majina hayo Kamati ya Ufundi ya TOC itakayokutana Jumamosi itachukua jukumu hilo
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa