Tathmini ya huduma za afya katika Zahanati na Hospitali za
Manispaa ya Kinondoni inaonyesha kuwa, kutokuwapo na mawasiliano
miongoni mwa mamlaka za Serikali kumechangia kutokea kwa hasara ambazo
zingeweza kuepukika.
Akiwasilisha ripoti ya tathmini iliyofanywa na
Sikika chini ya Mradi wa ufuatiliaji na uwajibikaji kwa jamii (SAM),
Mwenyekiti wa mradi huo, Alex Mwidima alisema majengo mengi ya zahanati
za manispaa hiyo yalijengwa bila kupimwa hivyo kutakiwa kubomolewa.
Alitoa mfano wa zahanati ya Wazo ambayo inatakiwa
kuvunjwa ili kupisha bomba la Maji la Dawasco ikiwa ni matokeo ya jengo
hilo kujengwa bila kupimwa.
“Pamoja na changamoto kadhaa, tumegundua hospitali
na zahanati nyingi ndani ya manispaa zimejengwa bila kupimwa na matokeo
yake hasara kutokana na nyingi kutakiwa kubomolewa,” alisema Mwidima
Aidha ripoti hiyo imebainisha matumizi fedha tofauti na maelekezo yaliyotolewa kwa kazi husika.
Akiwasilisha sehemu ya tamthimi hiyo, Samwel
Mhando ambaye ni Mjumbe wa SAM aliitaja Hospitali ya Mwananyamala
kupatiwa Sh31.8 milioni kwa mwaka 2011/2012 kwa ajili ya upanuzi wa
chumba cha kuhifadhia maiti, lakini fedha hazikutumika kama
ilivyokusudiwa.
Kwa mujibu wa Mhando hakuna upanuzi wowote
uliofanyika katika hospitali hiyo, huku vitabu vya manispaa vikionyesha
fedha hizo tayari zimeshatolewa.
Alisema fedha hizo zilitolewa ili kupanua chumba hicho ili kiweze kuchukua miili 50 badala ya 15.
Akijibu kuhusiana na hilo Mratibu wa Mipango ya
Afya Manispaa ya Kinondoni, Dk Ezra Ngereza alisema hospitali ilifikia
uamuzi wa kusogeza mradi wa upanuzi wa chumba hicho kwa sababu maalumu.
“Kulikuwapo malalamiko ya Waislamu na Wakristo kupinga maiti kuoshwa
chumba kimoja, hivyo fedha hizo zitumike kujenga vyumba viwili.”
alisema.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment