Dar es Salaam.Muunganiko wa wadau wa afya umeitaka Serikali na
wajumbe wa Bunge la Katiba kuweka suala afya kama mojawapo ya haki za
msingi za Watanzania.
Na kwa sababu hiyo, wameshauri Bunge kuhakikisha linasimamia mabadiliko kwa masilahi ya taifa.
Na kwa sababu hiyo, wameshauri Bunge kuhakikisha linasimamia mabadiliko kwa masilahi ya taifa.
Akizungumza wakati wa kutoa tamko hilo la wadau wa
afya lililohusisha asasi ya Sikika, Chama cha Madaktari(MAT), Kituo cha
Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) na Chama cha Afya ya Jamii, Mkuu wa
Program ya Sikika Josephat Mshighati alisema hatua hiyo imefikiwa baada
ya kuona Rasimu ya Katiba haijazungumzia kwa undani kuhusiana na suala
la afya.
Alisema licha ya kukutana na kupeleka maoni yao
kwa wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kutaka afya iwe mojawapo ya
haki za msingi za Mtanzania ,suala hilo halikuzingatiwa ingawa lina
umuhimu mkubwa kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi.
“Tumeona rasimu imegusia kuhusiana na suala la
afya, lakini hakuna kifungu kilichojadili kwa undani hivyo jambo hili
linaonekana kama kitu cha kawaida.”
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment