Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Kampuni ya Intertechnology Ltd ya Dar es Salaam, imeanza kuuza
na kukopesha matrekta yenye gharama nafuu kwa wakulima kwa lengo la
kuongeza kasi ya mapinduzi ya kijani katika sekta ya kilimo.
Mbali na hayo, pia kampuni hiyo imesema
inatekeleza sera ya kilimo kwanza kwa kuhakikisha kila mwananchi anapata
uhakika wa kuongeza kipato kupitia kilimo.
Kauli hiyo ilitolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji
wa kampuni hiyo, Dk. Francis Mayaka wakati akizindua matrekta hayo
yaliyotengenezwa nchini Belarus yenye ukubwa wa injini HP40 mpaka 320.
Dk. Mayaka alisema kuwa kila trekta litauzwa
kuanzia kiasi cha Sh30 milioni hadi Sh35 milioni ili kuwafikia
Watanzania wengi kwa lengo la kuhakikisha kila mmoja anakuza uchumi
kupitia sekta ya kilimo.
“Tumelenga kila mkulima nchini apate fursa ya
kununua trekta la kisasa kwa bei nafuu kuanzisha ukubwa wa injini HP40
hadi HP320 tofauti na baadhi ya matrekta mengi yaliyopo nchini sasa
yenye uwezo wa injini kuanzia HP40 hadi HP60.” alisema
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment