Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
CCM
Mhadhiri wa Shule Kuu ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
(UDSM), Jesse James , alisema hayo alipoulizwa na NIPASHE kuhusu sababu
za CCM kuhofia kuwa serikali tatu zitavunja Muungano.
“Ninachokiona kama hoja ya CCM ambayo hawaisemi kwa kina pengine
wanaogopa kugawa madaraka maana ukiwa na serikali tatu hakuna Rais
atakayekuwa na nguvu kama ilivyo Rais wa sasa.” Alisema Jesse.
Alifafanua kuwa hofu hiyo pengine inatokana na uwezekano wa chama
zaidi ya kimoja kushinda uchaguzi na kushika dola,hivyo inawezekana
vyama vitatu vikaongoza nchi.
Alisema CCM mathalani naweza kushinda kwenye uchaguzi wa serikali
ya Muungano, Chadema wakachukua ushindi serikali ya Tanganyika na
pengine CUF ikashinda na kuchukua serikali Zanzibar.
Hata hivyo, alisema haoni sababu kwanini Muungano uvunjike na
kueleza kuwa anaamini kuwa kabla ya kuuvunja wananchi wataangalia faida
na hasara zake ni jambo ambalo halina haja ya kuwaletea hofu Watanzania.
“Pengine kama viongozi hawatakuwa na nia njema wanaweza kuleta
mtafaruku na kuvunja Muungano,” alionya. Jesse alisema CCM walitakiwa
kueleza kile wanachosema muundo wa serikali wanaoutaka ni wa serikali
mbili zilizoboreshwa.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment