Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Saada Mkuya, Waziri wa fedha
Hayo yalibainishwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha
Utendaji katika Wizara ya Fedha, Emmanuel Tutuba, wakati akielezea
kuhusu utaratibu wa wizara katika kutekeleza BRN.
Tutuba alisema malengo ya wizara yake ni pamoja na kupunguza nakisi
ya bajeti na kutafuta mapato ya ziada kiasi cha Sh. Trilioni 3.8 kwa
miaka hiyo.
Alisema lengo lingine ni kutekeleza miradi ya ushirika wa pamoja kati ya sekta binafsi na Umma (PPP).
Tutuba alisema serikali imelenga kushirikiana na sekta binafsi
katika kutekeleza miradi ya kimkakati yenye thamani ya Sh. Trilioni 6
hadi ifikapo mwaka 2015/16. Alisema miradi ya awali ambayo imebainishwa
kuanza kutekelezwa kwa ubia huo ni ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam
hadi Chalinze.
Miradi mingine ni uendeshaji wa mradi wa mabasi yaendayo haraka Dar
es Salaam na ujenzi wa kituo cha kufua umeme cha kinyerezi 111. Pia
alisema utekelezaji wa viashiria vya kudhibiti matumizi ya serikali
utazingatiwa katika bajeti ya mwaka wa fedha 2014/15 kama ilivyopangwa
wakati wa uchaguzi wa kimaabara wa BRN.
Kuhusu kutoa fedha katika wizara zinazotekeleza BRN, alisema wizara
yake itaendelea kutekeleza jukumu la kutafuta na kutoa fedha za
kugharamia shughuli za utaratibu huo.
Alisema katika kipindi cha mwezi Julai hadi Disemba mwaka jana
wizara yake ilitoa fedha za maendeleo kwenye wizara zinazotekeleza mradi
huo. Alitaja miradi hiyo kuwa ni elimu ambayo ilipewa Sh. Bilioni 8.3,
maji Sh. Bilioni 86.0, kilimo Sh. Bilioni 10.2, uchukuzi Sh. Bilioni
146.6 na nishati Sh. Bilioni 339.4.
Kadhalika alisema kati ya Julai/Disemba mwaka huo jumla ya Sh.
Bilioni 10.9 zilikusanywa kutokana na utekelezaji wa hatua za BRM za
kuongeza mapato yasiyo ya kodi.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment