Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Katibu Mkuu Wizara ya Maji, Mhandisi Bashir
Mrindoko (katikati), akiwaeleza wafadhili wakuu wa mradi wa Maji Yetu,
Eric Beaune, kutoka Umoja wa Ulaya (EU) (kushoto) na Peter Moors, kutoka
Ubiligiji baada ya uzinduzi wa visima vya mradi wa maji katika shule za
msingi Mbagala Kuu jijini Dar es Salaam.
Miradi hiyo ipo 15 ambayo inalenga kuwanufaisha wananchi 170,000 katika wilaya ya Ilala ambayo itakuwa na miradi mitano, Kinondoni muradi minne na Temeke miradi sita.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Bashiru Mrindoko alisema mradi hiyo ni mkubwa na kuwataka wananchi kuitunza kwani itasaidia kwa kiwango kikubwa kutatua tatizo la maji jijini humo.
Alisema wizara yake imetengewa bajeti ya Sh. bilioni 10.7 kwa ajili ya sekta ya maji na itasaidia kutatua tatizo la maji kwa asilimia 50 jiji Dar es Salaam.
"Huu mradi wa maji ni zaidi ya bajeti yetu ya fedha tunazopatiwa hivyo ni lazima miundombinu itunzwe kwa umakini na yule atakayebainika kuhujumu atawajibishwa kwani atakuwa ana hujumu uchumi," alisema.
Aidha, alisema atalishughulikia tatizo la umeme ili kuepukana na matumizi ya diseli katika majenereta yatakayotumika katika mitambo ya maji, kwani bila hivyo watajikuta wakitumia gharama kubwa katika uendeshaji wa miradi hiyo.
Naye Balozi wa Ubelgiji nchini, Koenraad Adam alisema lengo la mradi huo ni kusaidia familia ili ziweze kuishi katika mazingira bora.
Alisema bila maji safi hakuna maisha bora kwa wananchi hivyo wananchi wanatakiwa kusimamia viwango vya usafi na kutunza mazingira yanayoizunguka miradi hiyo.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment