Home » » ‘Washtakiwa EPA wana kesi ya kujibu’

‘Washtakiwa EPA wana kesi ya kujibu’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu imewaona wakurugenzi wa kampuni ya Njake Hotel &Tours, Jonathan Munisi na Japhet Lema wanaokabiliwa na kesi ya wizi kwenye akaunti ya EPA, kuwa wana kesi ya kujibu katika mashtaka yote yanayowakabili.
Katika kesi hiyo, kampuni hiyo ya Njake Hotel & Tours inadaiwa kuchota Sh.22 bilioni kutoka akaunti hiyo kiasi hicho cha fedha kwa madai ilirithishwa deni hilo na Kampuni ya E.Itoh ya Japan.
Uamuzi huo ulitolewa jana na jopo la mahakimu watatu linaloongozwa na Jaji Beatrice Mutungi baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano walioitwa na upande wa mashtaka pamoja na vielelezo vilivyowasilishwa kama sehemu ya ushahidi kwenye kesi hiyo. Baada ya uamuzi huo kutolewa, washtakiwa waliiambia mahakama kuwa watatoa utetezi wao kwa njia ya kiapo. Mshtakiwa wa kwanza aliieleza mahakama kuwa ataita shahidi mmoja wa kumtetea huku mshtakiwa wa pili akijitetea mwenyewe.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 27,2014 wakati washtakiwa hao watakapoanza kutoa ushahidi wa utetezi dhidi ya mashtaka yanayowakabili.
Aprili 13, 2011,Mfanyakazi  wa Benki ya NBC, Lyson Mwakapenda (67),  akitoa ushahidi  katika kesi hiyo, aliieleza Mahakama kuwa benki hiyo, ilizirejesha fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT), baada ya kuziona kuwa ni mzigo kufuatia kukaa nazo kwa kipindi kirefu. Mwakapenda alidai kuwa yeye ndiye aliyesimamia malimbikizo ya fedha za EPA yaliyotokana na fedha za kigeni zilizolipwa na wafanyabiashara walioagiza bidhaa zao kutoka nje ya nchi.
Alidai kuwa baada ya uhaba wa fedha za kigeni, Benki ya NBC ililazimika kufungua akaunti hiyo ya EPA. Aliendelea kudai kuwa Benki ya NBC ilikaa na fedha hizo kwa kipindi kirefu kiasi cha kuonekana kuwa ni mzingo na hivyo NBC iliamua kuzirejesha BoT baada ya Hazina na BoT kukubaliana kuhusu kuhamisha fedha hizo kutoka katika matawi ya NBC kwenda kwenye akaunti ya EPA. Alidai kuwa NBC, ilifanya kazi hiyo kwa maelekezo kutoka BoT.
Chanzo;mwananchi

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa