Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Rais Jakaya Kikwete anatarajia kuongoza mkutano wa mashauriano
ya awamu ya kwanza ya uwekezaji katika mradi wa mabasi yaendayo kasi
(DART) utakaowakutanisha wawekezaji wa ndani na nje Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa DART, Asteria Mlambo alisema
mwishoni mwa wiki kuwa mkutano huo utakaofanyika mapema mwezi ujao
utatoa nafasi kwa wawekezaji kuzijua fursa za uwekezaji zitakazopatika
kwenye mradi huo.
Washiriki wa mkutano huo wanatarajiwa kutoka
katika benki na taasisi mbalimbali za kifedha, kampuni za kutengeneza
mabasi, kampuni za mawasiliano, mifuko ya kijamii na wengine.
Mada kuhusu mradi wenyewe wa DART itatolewa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Tamisemi), Jumanne Sagini.
Kabla ya mkutano huo, DART imeandaa mkutano wa
wamiliki wa daladala Dar es Salaam, Kampuni ya Usafirishaji Dar es
Salaam (UDA) na wadau wengine ili kuwafahamisha jinsi gani wanaweza
kunufaika na mfumo huo mpya.
“Tutawaelezea faida na fursa zitakazopatikana kwenye mfumo mpya wa usafirishaji jijini,” alisema Mlambo.
Mwezi uliopita Dart ilikamilisha shughuli ya
kusajili mabasi ya daladala yanayopita katika Barabara ya Morogoro au
kukatiza katika njia hiyo ikiwa ni moja ya matayarisho ya kupisha mradi
huo.
Kulingana na mpango huo wa Dart barabara hizo za
Morogoro, Kawawa na Msimbazi zitatumiwa na mabasi ya mfumo huo pekee kwa
njia 64 Dar es Salaam zitakoma kutumika kutokana na mradi huo.
Chanzo:Mwananchi
Chanzo:Mwananchi
0 comments:
Post a Comment