Mkaguzi
na mdhibiti mkuu wa hesabu za serikali Bwana Ludovick Utouh akikmabidhi
Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete Tuzo maalum kwa kutambua mchango wange
kwa taasisi simamizi katika kuimarisha Uwazi,Uadilifu na uwajibikaji
wakati wa hafla maalum ya chakula cha jioni iliyofanyika katika ukumbi
wa wa kimataifa wa mikutano Julius Nyerere(JNICC) jijini Dar es Salaam
Bwana
Utouh alikabidhi Tuzo hiyo kwa niaba ya taasisi sita ambazo ni Bodi ya
Taifa ya wahasibu na wakaguzi,TAKUKURU, Mamlaka ya Udhibiti na Ununuzi
wa Umma, Mamlaka ya udhibiti wa Mifuko ya Hifadhi ya jamii, Mkaguzi wa
ndani Mkuu wa Serikali na Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa umma
(picha na FreddyMaro).
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
ametaja misingi mikuu mitano ambayo utekelekezaji wake unathibitisha
kushamiri kwa utawala bora nchini.
Aidha, Rais
Kikwete amesema kuwa pamoja na kwamba utawala bora unaendelea kushamiri
nchini, bado taasisi za usimamizi wa masuala ya utawala bora zina
nafasi ya kuboresha kazi yao na kupanua kwa kiasi kikubwa zaidi utawala
bora.
Rais
Kikwete aliyasema hayo usiku wa juzi, Jumatatu, Juni 23, 2014, wakati
alipozungumza baada ya kuwa ametunukiwa Tuzo ya Kutambua Mchango Wake wa
Kuimarisha Utawala Bora nchini ambayo imetolewa na taasisi nane za
usimamizi nchini.
Taasisi
hizo ni Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi, Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi
wa Hesabu (NBAA), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCB),
Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya
Jamii (SSRA), Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali (ACCGen-D), Ofisi ya
Mkaguzi Mkuu wa Serikali (IAG-D) na Sekretarieti ya Tume ya Maadili.
Hiyo ni
mara ya kwanza kwa Tuzo hiyo kutolewa nchini na ilikabidhiwa kwa Rais
Kikwete wakati wa chakula cha usiku kilichoandaliwa kwa ajili ya wajumbe
wa Mkutano wa Mwaka wa Wakaguzi wa Hesabu za Serikali kwenye Ukumbi wa
Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNICC) mjini Dar Es salaam.
Mkutano huo
wa mwaka pia unahudhuriwa na wajumbe waalikwa kutoka nchi za Ujerumani,
Afrika Kusini, Uganda, Sweden, Sierra Leone, Nigeria, Niger, Ghana,
Kenya, Zambia, Rwanda, Burundi na Ethiopia.
Akizungumza
baada ya kukabidhiwa Tuzo hiyo na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali (CAG) Bwana Ludovick Utoh, Rais Kikwete alisema kuwa Tanzania
ina utawala bora kwa sababu inadumisha misingi yote mikuu ya utawala
bora.
Aliitaja
misingi hiyo kuwa ni kushamiri wa demokrasia, uhuru wa kutoa maoni na wa
vyombo vya habari, haki ya kila Mtanzania kuishi, utawala wa sheria,
kutoingiliana kwa mihimili mitatu ya Serikali.
Rais
Kikwete ambaye amesema kuwa amepokea Tuzo hiyo kwa niaba ya viongozi
wenzake katika Serikali – Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri, Wakuu
wa Mikoa, Katibu Mkuu Kiongozi, Makatibu Wakuu na Wakuu wa Vyombo vya
Ulinzi na Usalama – amesema kuwa utawala bora ni jambo muhimu na halina
mbadala wake.
“Tanzania
tumeruhusu uhuru mkubwa kwa wananchi wetu kushiriki katika shughuli
zao. Serikali yetu haitishi watu wake. Hatufanyi hivyo. Ziko nchi
zinaishi kwa kutisha raia wake na nyie mnazijua, “ alisema Rais Kikwete.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
IKULU
DAR ES SALAAM
24 Juni, 2014
0 comments:
Post a Comment