Home » » MSIKITI MTAMBINI WAUNGUA MOTO

MSIKITI MTAMBINI WAUNGUA MOTO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Gari la kikosi cha Zima moto likiwa katika msikiti wa Mtambani katika harakati za kuzima moto huo iliowaka majira ya saa moja usiku jana
 
Moto umezuka katika msikiti wa Mtambani uliopo wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam na kuzua taharuki kubwa miongoni mwa waumini, majirani na wapita njia.
Tukio hilo limetokea jana majira ya jioni na kusababisha mamia ya wananchi kujitokeza kusaidia kuuzima kabla ya vikosi vya zima moto kuwasili eneo la tukio.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo baada ya kuzungumza na NIPASHE akiwa eneo la tukio.

Hata hivyo, chanzo cha tukio hilo bado hakijajulikana na hadi tunakwenda mitamboni,  vikosi mbalimbali vya zimamoto kutoka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam vilikuwa vikiendelea kuuzima moto huo.

Msikiti huo pia una shule za sekondari na msingi za Mivumoni.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported byBlogs za Mikoa
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa