Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » VURUGU KUBWA ZA DALADALA, BAJAJ ZAIBUKA DAR

VURUGU KUBWA ZA DALADALA, BAJAJ ZAIBUKA DAR

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillus Wambura
Vurugu kubwa vimeibuka jijini Dar es Salaam kati ya madereva daladala na bajaj huku sialaha za jadi zikitumika.
Vurugu hizo zilizopelekea bajaj mbili kupasuliwa vioo na dereva mmoja wa bajaji kujeruhiwa, zilizotokea Kimara Mavurunza katika kituo cha daladala cha Baa mpya. 
 
Aidha, hali hiyo imepelekea baadhi ya madereva wa daladala kushikiliwa katika kituo cha polisi Mbezi Kimara.
 
Kwa miaka kadhaa kumekuwapo na shida ya usafiri kwa kwa abiria watokao Kimara Mwisho kuelekea Kimara Bonyokwa kutokana na njia kuwa mbaya, hali inayo changia wamiliki wa vyombo vya abiria kushindwa kupeleke vyombo vyao katika maeneo hayo.
 
Kutokana na hali hiyo, baadhi ya daladala zisizo kuwa na vibali vya kutembea barabarani, ndizo zimekuwa zikisafirisha abiria kutoka Kimara Mwisho kuelekea Bonyokwa.
 
Hivi karibuni bajaj zimeanza kutoa huduma za kusafirisha abiria kutoka Kimara-Bonyokwa kwa nauli ya Sh. 1,000 na kusababisha baadhi ya madereva wengi wa daladala kuwafanyia vurugu wenye bajaj.
 
Mwenyekiti wa madereva bajaj Kimara, John Muhuni, alisema fujo hizo zilisababishwa na madereva wa daladala kujifanya kuwa wao ndio wenye njia hiyo.
 
“Tumeanza kubeba abiria hapa huu ni mwaka wa pili, kila wakati wamekuwa wakitufanyia fujo, tunafikisha taarifa polisi, lakini hakuna hatua zinazochukuliwa,”alisema Muhuni. 
Aliongeza kuwa baada ya kuona hivyo waliamua kupeleka taarifa katika uongozi wa serikali za mitaa na juzi waliamua kuwakutanisha.
 
 
Muhuni aliongeza baada ya kukutana walikubaliana kila mtu apakie abiria kupeleka katika kituo cha Baa Mpya.
“Lakini toka jana (juzi),wenzetu wamekuwa wakijiandaa kutufanyia fujo,”alisema.
 
 Jacqueline Makalu, Makamu Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa ya Kimara Bonyokwa alisema fujo hizo zilianza saa 1:00 asubuhi na kumalizika saa 3:00 asubuhi baada ya polisi kuwasili.
Aliongeza kuwa madereva wa daladala wamekuwa wakorofi kwa muda mrefu na kwamba kwa sasa wamewawekea sheria ambayo itawadhibiti.
 
Dereva wa daladala, Kasimu Masumbuko, alisema wamekuwa wakiwaomba bajaj kuacha kupakia abiria kwa,kuwa wanawachukulia wateja wao, lakini wenzao wanawapuuza.
 
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Camillus Wambura,  alidhibitisha kutokea kwa tukio hilo huku na kusema uchunguzi unaendelea kubaini wahusika.   
 
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa