Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » ‘WANAFUNZI SOMENI FANI ZENYE FURSA’

‘WANAFUNZI SOMENI FANI ZENYE FURSA’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira, imeandaa mpango wa kutoa elimu kwa wanafunzi wa vyuo mbalimbali, ili kuwajenga wasomee fani zenye fursa za ajira.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Ofisa Habari Mkuu wa Sekretarieti ya Ajira, Riziki Abraham alisema mkakati huo unalenga kupunguza tatizo la ajira.
“Ukweli ni kwamba, ajira zimekuwa za ushindani kwa sababu vyuo vimekuwa vingi, lakini kuna programu tumeanzisha ya kuwahamasisha wanafunzi kutojenga dhana ya kuajiriwa pekee au kung’ang’ania fani zisizokuwa na soko,” alisema Abraham na kuongeza: “Sisi kazi yetu ni kuwashauri, hivyo chini ya programu hii tunalenga kuwashawishi wasome kulingana na mahitaji ya soko la ajira.”
Pia alitumia fursa hiyo kuwaonya watumishi wa umma, hasa wanawake ambao wamekuwa na tabia ya kubadilisha majina kiholela pindi wanapoolewa.
“Sekretarieti ya Ajira, inawataka wote waliobadili majina kwa sababu mbalimbali iwe ya kidini, kuolewa au kutopenda yale ya utotoni na kuwa na majina tofauti kwenye vyeti, wafuate sheria,” alisisitiza.
Alifafanua kuwa siyo vibaya kwa mwanamke kubadili jina na kutumia jina la ubini wa mumewe, ingawa pia wapo ambapo wamejikuta katika wakati mgumu baada ya ndoa zao kuvunjika, hivyo kuhangaika kubadilisha majina kwa mara nyingine.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa