Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
amemteua Bwana Lusekelo Mwaseba (pichani) kuwa Naibu Kamishna Mkuu wa
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Taarifa
iliyotolewa Ikulu, Dar Es Salaam, leo, Jumatano, Oktoba Mosi, 2014, na
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, imesema kuwa uteuzi huo
unaanza leo.
Kabla ya uteuzi wake, Bwana Mwaseba alikuwa Kamishna wa Uchunguzi katika Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Imetolewa na;
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu – Dar es Salaam.
1 Oktoba, 2014.
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment