Mkurugenzi Mtendaji Tanesco, Felchesmi Mramba.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Naibu Mkurugenzi wa Tanesco, Decklan Mhaiki, alisema shirika lake linaomba radhi kwa usumbufu huo uliojitokeza.
“Tunaomba radhi kwa usumbufu huo na kwamba kwa sasa tatizo limeshashughulikiwa kwa asilimia 70(jana) na hadi kufikia kesho (leo) tatizo hilo loitakuwa limekamilika kwa asilimia 100…mafundi wetu wanaendelea na matengenezo ili kumaliza kero hiyo,” alisema Mhaiki.
Naye Meneja Mwandamizi wa Tehama (ICT), Kusenha Mazengo, alisema tatizo hilo lilikuwa katika mifumo ya kusambaza umeme wa luku kwenda kwa mawakala wanaosambaza kwa wateja wa kawaida.
“Wateja wetu walikosa huduma hiyo kutoka kwa mawakala kutokana na hitilafu ya mfumo huo, “ alisema Mazengo.
Mapema Januari 10, mwaka huu mfumo wa luku ulishindwa kufanyakazi na kusababisha baadhi ya watu kukosa huduma ya nishati hiyo.
CHANZO:
NIPASHE
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
0 comments:
Post a Comment