Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » SERIKALI YATAHADHARISHA MATUKIO YA UHALIFU ULIOPITILIZA MIPAKA

SERIKALI YATAHADHARISHA MATUKIO YA UHALIFU ULIOPITILIZA MIPAKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), imetahadharisha kuwapo na matukio machache yenye dalili za uhalifu uliopitiliza mipaka yanayohusisha kuua wanajeshi pamoja na polisi.
 
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, aliliambia Bunge jana, wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka 2015/16.
 
Alisema licha ya hali ya usalama wa taifa kuwa ya kuridhisha kuna matukio kama hayo ya kuwaua askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na polisi na kuwapora silaha vituoni akisema  ni udhihirisho wa uhalifu uliopitiliza.
Akizungumzia usalama mipakani alisema ni shwari japo kwa upande wa Magharibi wahalifu wenye silaha wanaodhaniwa kutokea Congo na Burundi, walivamia,  kushambulia  na kupora  wavuvi kwenye Ziwa Tanganyika na Victoria.
 
Kwa upande wa  mipaka Kusini alieleza kuwa licha ya kwamba kuna mgogoro baina ya Malawi na Tanzania kuhusu mpaka wa Ziwa Nyasa eneo hilo liko salama .   
 
WASIOKWENDA JKT KUBANWA
Waziri aliliambia Bunge kuwa idadi ya waliojiunga na JKT katika mwaka 2014/15 ni 40,082, hata hivyo, aliwaonya wale ambao hawakwenda kwa mujibu wa sheria wataendelea kuhesabika kama watoro.
“Wito wangu kwa vijana ni kushiriki mafunzo haya kwani ni ya mujibu na kwa wale ambao hawakushiriki bila ridhaa yetu wataendelea  kuwa kwenye orodha yetu ya vijana watoro,” aliliambia Bunge.
 
KUZALISHA MILIPUKO
Akizungumzia uzalishaji jeshini alisema Shirika la Mzinga, linakusudia kuanzisha kiwanda cha milipuko pamoja na kituo cha utafiti wa zana za kivita.
 
Waziri wa Ulinzi alisema pamoja na kuanzisha vituo hivyo Mzinga itasimika mfumo wa  usalama wa  kielektroniki katika kiwanda hicho.
Alisema shirika hilo katika mwaka  wa fedha wa 2014/15 liliendelea kukamilisha ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha risasi  na kukarabati  na kujenga maghala  mapya ya silaha.
CHANZO: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa