Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » NI MSIBA TENA JAMBO CONCEPTS (T) LTD, WACHAPISHAJI WA GAZETI LA JAMBO LEO

NI MSIBA TENA JAMBO CONCEPTS (T) LTD, WACHAPISHAJI WA GAZETI LA JAMBO LEO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya Jambo Concepts (T) Ltd, inayochapisha magazeti ya Jambo Leo, Staa Spoti na Jarida la Jambo Brand, limempoteza mfanyakazi wake mwingine wa idara ya masoko, Kinai Mtinda (pichani), baada ya kufariki dunia saa 7 usiku wa kuamukia leo katika Hospitali ya Sinza Palestina jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa kwa matibabu.

Msiba na mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa kaka yake Mbezi Beach na taratibu zingine kuhusiana na msiba huo zitatolewa baadae.

Marehemu Kinai ameacha watoto wawili.

Kifo cha Mtinda kinakuja ikiwa ni siku chache tangu afariki dunia Meneja Mkuu wa Kampuni hiyo, Ramadhani Kibanike mwishoni mwa mwezi uliopita. Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake libarikiwe Amina.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa