Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Naibu waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba
ameonesha kushangazwa na mfanano wa vichwa vya habari vya magazeti ya
leo kuhusu mgombea urais wa Chadema, Edward Lowassa.
Makamba ambaye ni mjumbe wa kamati ya kampeni ya CCM, ameonesha kurasa
za mbele za magazeti ya Mtanzania, Mwananchi na Tanzania Daima
zilizokuwa na vichwa vya habari vinavyomnukuu Lowassa akitaka watanzania
wasiogope.
Amepost picha za magazeti hayo kwenye twitter na kuhoji kama mfanano huo ni bahati mbaya au imeratibiwa.
0 comments:
Post a Comment