Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na
Ally Daud-MAELEZO
Jopo
la Elimu ya Kiislamu nchini (IEP) limetangaza matokeo ya wanafunzi waliofanya mtihani
wa dini hiyo wa kuhitimu darasa la saba Agosti 12 mwaka huu.
Kauli
hiyo imetolewa na Afisa Mwandamizi wa jopo hilo Bw. Suleimani Daud alipokuwa
akiongea na Waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.
Bw.
Suleimani amesema kuwa wanafunzi ambao walifanya mtihani huo idadi yao ilikuwa 86,613
kati ya wanafunzi 93,101 waliojisajili nchini kutoka shule 3094 ambazo wanafunzi
walifanya mtihani huo mwaka 2015 zaidi ya wanafunzi 2559 kutoka shule mwaka 2014.
Idadi
za hiyo ya wanafunzi imeongezeka kutokana na ongezeko la wilaya zilizoshiriki katika
mtihani huo kutoka Wilaya 115 kwa mwaka 2014 hadi kufikia Wilaya 127 mwaka huu ambazo ni sawa na asilimia 10.4.
Aidha
Bw. Daud amesema kuwa kiwango cha ufaulu kimepungua kutoka wastani wa 46.45
mwaka jana hadi kufikia wastani wa 40.1 sawa
na asilimia 13.67 mwa huu.
Mtihani
ulikuwa na jumla ya alama asilimia 100 wastani wa ufaulu kitaifa ni asilimia
13.67 ambao umepatikana kwa kutafuta wastani huo wa kila mkoa na kugawa kwa idadi
ya mikoa yote nchini.
0 comments:
Post a Comment