Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Serikali imekiri
kwamba CT Scan mpya iliyonunuliwa kuziba pengo la kuharibika kwa
iliyokuwepo katika hospitali ya Muhimbili Dar es salaam ilitolewa
hospitali ya Benjamin Mkapa Ultra modern Hospitali mkoani Dodoma
Hayo yamebainika leo
katika ukumbi wa bunge mjini Dodoma baada ya Mbunge wa jimbo la Chemba
Juma Nkamia CCM kuuliza swali kwanini serikali imeamua kuchukua mashine
ya CT Scan katika hospitali inayohudumia wagonjwa Dodoma na kuipeleka
Muhimbili ina maana serikali ina lengo la kuwaua wananchi wa Dodoma.?
Akijibu swali hilo
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt.
Khamisi Kigwangalla amesema kwamba serikali ilichukua uamuzi huo baada
ya mashine hiyo kukosa jengo la kuifunga Mkoani Dodoma ambapo wakati huo
huo hospitali ya Muhimbili imekuwa ikiwa inakumbwa na matatizo makubwa
ya wagonjwa kukosa huduma hiyo.
''Mheshimiwa
mwenyekiti kwa kuwa hospitali ya Benjamin Mkapa Ultra modern ilipata
mashine hiyo lakini jengo lao bado halikamilika hivyo serikali imeandaa
utaratibu wa kununua mashine mpya kwa ajili yao ili jengo lao
likikamilika liweze kupata mashine mpya'' Ameeleza Dkt.Kigwangalla.
0 comments:
Post a Comment