Sikiliza Tone Radio Live Hapa, na Tembelea Website yetu www.toneradiotz.com
Home » » MAMA MAGUFULLLI ASAIDIA WASIOJIWEZA.

MAMA MAGUFULLLI ASAIDIA WASIOJIWEZA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mke wa Rais, Mama Janeth Magufuli (wa pili kushoto) akikabidhi mchele, unga kili 6000 na maharage kilo 1200 kwa Mwenyekiti wa Kituo cha Wazee na Walemavu wasiojiweza cha Nunge Vijibweni Kigamboni Manispaa ya Temeke Dar es Salaam, Anthony Kikongoti (wa pili kulia), jana. Kulia ni Afisa Mfawidhi wa kituo hicho, Ojuku Mgedi na Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Temeke Sophia Mjema. (Picha na Ikulu).
MKE wa Rais, Mama Janeth Magufuli amesema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha wazee na watu wasiojiweza wanapata huduma zote muhimu kwa kadri ya uwezo wake.
Aliyasema hayo jana Dar es Salaam wakati alipofanya ziara yake ya kwanza ya kikazi katika Kituo cha makazi ya wazee na watu wenye ulemavu cha Nunge, Kigamboni katika Manispaa ya Temeke na kuwakabidhi zawadi ya vyakula.
“Serikali ina wajibu mkubwa katika kuhudumia wazee na watu wasiojiweza lakini mtakubaliana kuwa serikali pekee haiwezi kumaliza matatizo yote yanayowakabili watu hawa. Hivyo sote kwa pamoja tuna wajibu wa kusaidia nguvu za serikali katika kuwahudumia wenzetu hawa,” alisema.
Alisema kwa kulitambua hilo ametoa mchele kilo 3,000, unga kilo 3,000 na maharage kilo 1,200, ambavyo kulingana na idadi yao kila mmoja amepatiwa kilo 25 za mchele, kilo 25 za unga na kilo 10 za maharage.
“Sote tunafahamu kuwa wazee na watu wasiojiweza wanahitaji upendo, kuthaminiwa na kusaidiwa na kipimo kimoja wapo cha kupima jamii iliyostaarabika na inayoheshimu misingi ya utu ni kuangalia namna inavyowathamini wazee na watu wasiojiweza,” alieleza mke huyo wa Rais Magufuli.
CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Dar es salaam Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa