Na Immaculate Makilika- MAELEZO
Serikali imetangaza rasmi alama za Jumuiya ya Afrika Mashariki zitakazotumika kwenye Ofisi za Serikali na katika shughuli zote rasmi za kiserikali.
Mkuu
wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini wa Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa Bi. Mindi Kasiga
amezitaja alama hizo kuwa ni bendera ya Taifa,bendera ya Jumuia ya
Afrika Mashariki, wimbo wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wimbo wa
Taifa.
Kasiga amewambia waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuwa, kuanzia sasa bendera ya Jumuiya hiyo itapepea
sambamba na Bendera ya Taifa kwenye Ofisi zote za Serikali huku wimbo
wa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki ukiimbwa sambamba na wimbo wa Taifa
katika shughuli rasmi za serikali kuanzia ngazi za Halmashauri hadi
Taifa, ikiwa ni hatua ya utekelezaji wa Mkataba wa uanzishwaji wa
jumuiya hiyo kifungu cha 7(a).
“Mkataba
huu unasisitiza jumuiya hii kuwa jumuiya ya watu, hivyo watanzania
watahusishwa katika hatua zote za mtangamano huo, pamoja na
kushirikishwa kikamilifu katika hatua mbalimbali za jumuiya ili kujua
madhumuni ya kunufaika na fursa mbalimbali zitakazaopatikana ndani ya
Jumuiya hiyo”, alisema Bi. Kasiga
Aidha,
matumizi ya alama hizi ni njia mojawapop ya kujenga uzalendo na
kumfanya Mwananchi ajisikie kuwa sehemu ya ushirikiano huu, aliongeza
Bi. Kisiga
Vilevile, taasisi binafsi zinaweza
kutumia alama hizi, huku shule na vyuo vikisisitizwa kutumia alama hzi
kama sehemu ya kuelimisha na kuhamasisha vijana kuhusu Jumuiya ya Afrika
ya Mashariki.Wizara ya Mambo ya Nje, na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
inaratibu upatikanaji wa sampuli ya alama hizo kwa gharama za taasis,
wizara au Ofisi husika.
0 comments:
Post a Comment