Frank Mvungi
–Maelezo
Wanaharakati
na wanasiasa wanaobeza juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano, wametakiwa kuacha
kuupotosha umma juu ya mafanikio yaliyofikiwa na Serikali hiyo chini ya Rais
Dkt. John Pombe Magufuli.
Kauli hiyo
imetolewa Jijini Dar es salaam leo na Afisa Habari wa CZI- information And
Media Consults Co. Ltd, Augustino Matefu
wakati wa mkutano na vyombo vya Habari uliolenga kueleza mafanikio ya
Serikali ya awamu ya tano.
Alisema Serikali
ya awamu ya tano imeonesha mafanikio makubwa katika sekta ya ukusanyaji mapato,
elimu, miundombinu, afya na kujenga uwajibikaji miongoni mwa watumishi wa umma.
Hivyo alitoa
wito kwa Watanzania wote kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano na
kuwapuuza wanaharakati na wanasiasa hao wanaunga mkono wale wasioitakia mema Tanzania
na Serikali ya awamu ya tano kwa ujumla.
Alisema
katika sekta ya mapato, Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi cha miezi saba
iliyopita imefanikiwa kuongeza mapato kutoka shilingi bilioni 900 kwa mwezi kabla
ya utawala wake hadi shilingi trilioni 1.5 kwa sasa.
“Rais wa awamu ya tano ameondoa michango yote
ya shule za msingi na Sekondari ambayo ilikuwa kero kwa wazazi na wananchi kwa
ujumla” alisisitiza Matefu
Katika
mpango wa elimu bure Matefu alibainisha kuwa umesaidia kuongeza idadi ya
wanafunzi wanaoandikishwa kujiunga na elimu ya msingi na ile ya Sekondari.
Aliongeza
kuwa Rais Magufuli amejenga Barabara ya Mwenge hadi Moroko kwa Fedha za ndani
hali inayoonyesha kuwa Serikali inayo dhamira ya dhati ya kuwaletea
maendeleo wananchi wake.
Alisema hata
Hosipitali ya Taifa Muhimbili Kupatiwa vitanda
vya kutosha na hivyo kuondoa tatizo la msongamano katika wodi ya wazazi na kwa
sasa wagonjwa wanalala kwenye vitanda.
“Mambo
mengine yaliyofanywa na Serikali katika kipindi hiki yanalenga kuinua maisha ya
wananchi wa chini ikiwemo kujenga mazingira mazuri yatakayowezesha shughuli za
uzalishaji kuongezeka ili kuinua hali ya maisha ya wananchi” alisema Matefu.
Kujengwa kwa
utamaduni wa uwajibikaji miongoni mwa watumishi wa umma ni moja ya mambo
yaliyofanywa na Serikali ya awamu ya tano ambapo sekta ya utumishi wa umma
imeonesha mabadiliko makubwa katika uwajibikaji.
0 comments:
Post a Comment